Habari za Punde

Utata kifo cha bilionea aliefia gesti

Na Joseph Ngilisho, Arusha
UTATA umegubika kifo cha mfanyabishara bilionea,Olais Metili (65) mkazi Uzunguni jijini Arusha,aliyefia katika choo cha chumba alichokodi katika nyumba ya kulala wageni ya Diamond Motel, ambapo familia imeshindwa kueleza undani wa tukio hilo.

Aidha katika hali isiyokuwa ya kawaida wafanyabishara pamoja na majirani,waliususia msiba wa mfanyabiashara huyo,huku idadi ndogo ya vijana na familia ndio waliojitokeza nyumbani kwa marehemu.

Mdogo wa marehemu ambaye ndiyo msemeji wa familia,Onesmo Metili, alisema hawezi kuzungumzia suala hilo kwani tayari vyombo vya habari vinalifahamu.

“Mimi siwezi kuzungumzia suala hilo kwani vyombo vyenu vya habari vimeandika amekufa kwa viagra sasa mnataka niseme nini endeleeni kuamini hivyo,” alisema.

Mfanyabishara huyo alikutwa amekufa katika nyumba hiyo ya kulala wageni mwishoni mwa wiki, akidaiwa kumeza dawa ya kuongeza nguvu aina ya viagra baada ya kuingia na mwanamke kwa lengo la kustarehe,ambaye hakufahamika mara moja.


Taarifa kutoka vyanzo vvya habari katika nyumba hiyo, vimedai kwamba kwa muda mrefu marehemu amekuwa mteja wao na pindi anapokuja hupiga simu na kuwataka wamwandalie chumba na pindi anapomaliza kupumzika na mwenza wake hutoka na kurejea nyumbani kwake.

Siku ya tukio ilidaiwa kwamba marehemu alifika akiwa ameongozana na mwanamke mmoja na alipofika alikodi chumba na kuingia ndani,hata hivyo siku ya pili majira ya asubuhi,mhudumu mmoja aliingia katika chumba hicho kwa lengo la kukifanyia usafi ndipo alipopigwa na butwaa baada ya kukuta mwili wa mteja wao uko utupo ndani ya choo.

“Baada ya kuona mwili tulitoa taarifa kwa uongozi ambao walipiga simu polisi,hatukujua kama kulikuwa na mtu amekufa kwani ndani ya chumba kulikuwa hakuna mtu ila nilipojaribu kuingia chooni ndipo nilikuta yupo chini amekufa,” kilisema chanzo hicho.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ndugu wa merehemu,mwili wa mfanyabishara huyo utazikwa siku ya Ijumaa,kijijini kwao eneo la Ilboru baada ya taratibu zote za kuuaga  kukamilika.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.