Na Mwandishi wetu, Muscat
WAZIRI wa Habari, Utamaduni,
Utalii na Michezo Mhe. Said Ali Mbarouk, ameuelezea ushirikiano baina ya Oman
na Zanzibar kuwa daima utakuwepo na utaendelea kukua kutokana na kutanuka kwa
maeneo mapya ya ushirikiano katika nyanja mbali mbali za maendeleo.
Alisema ni jambo la faraja
kuona hivi sasa Zanzibar na Oman zinatambua umuhimu wa kutanua maeneo hayo ya
ushirikiano katika sekta za uchumi, utalii na michezo kwa lengo la kuwanufaisha watu wa pande zote mbili.
Aliyasema hayo kwa nyakati
tofauti wakati akizungumza na Mawaziri
wa sekta za Habari, Michezo, Utamaduni na Utalii mjini Muscat Oman jana akiwa
katika ziara yake ya siku nne ya kukutana na viongozi mbali mbali wa nchi hiyo
kwa lengo la kukuza ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.
Abdulmunim bin Mansoor bin Said
Al Hasani
Mapema akizungumza na Waziri wa
Habari wa Oman, Sheikh Dk. Abdulmunim bin Mansoor bin Said Al Hasani,alitoa
shukrani zake kwa serikali ya Oman kwa misaada yake kwa Zanzibar na kusifu
nidhamu ya vyombo vya habari vya nchi
hiyo katika kuwaunganisha watu na kuwawezesha kujenga uchumi imara.
Alisema hatua hiyo ya mfano wa kuigwa inatokana na usimamizi madhubuti
kwa vyombo vya habari na kujali kuwajibika kwa jamii kwa vile vinatoa
nafasi ya kuwapatia taarifa za kutosha juu ya harakati za kujiendeleza na
kujenga ustawi na maendeleo yao.
Alishauri haja ya kuwepo na
utaratibu wa kubadilishana wataalamu na vipindi ili kila nchi iweze kujifunza
kutoka upande mwengine kwa kutambua
maendeleo yanayofikiwa na kila upande na hivyo kutoa fursa za kuwawezesha
vijana na vyombo vya habari kuongeza kasi ya utekelezaji wa majukumu yao kwa
pamoja hasa kwa vile ni tegemeo kubwa la taifa katika kujenga uchumi.
Katika ziara yake hiyo,Waziri Mbarouk
pia alipata fursa ya kubadilishana mawazo na Naibu Waziri wa Utamaduni na Mambo
ya Kale, Sheikh Hamad Hilal Al Maamari na Waziri wa Michezo, Sheikh Shallal
Saad Mohammed Al Saad na kujikita zaidi
katika masuala ya kubadilishana wataalamu wa michezo na kuyahuisha majengo ya
kihistoria yenye mnasaba na Oman.
Wakati huo huo, ameiomba Oman kufungua fursa nyengine kwa kuisaidia
Zanzibar katika kuanzisha hoteli za kitalii za halali utaratibu ambao Oman
tayari imeuanzisha na kupata mafanikio.
Alisema utaratibu wa hoteli
kama hizo ni muafaka katika visiwa vya Zanzibar kwa vile zitaongeza soko la
idadi ya watalii wanaohitaji kupumzika katika maeneo yenye utulivu wa maadili
ya kidini na kiutamaduni.
Pia alipata fursa ya kushiriki
katika karamu rasmi iliyoandaliwa kwa
ajili yake na ujumbe wa watu watatu aliyofuatana na mwenyeji wake
Waziri wa Habari wa Oman, Sheikh, Dk. Abdulmunim bin Mansoor bin Said Al Hasani,iliyofanyika
katika jumba la serikali la Opera mjini Muscat.
No comments:
Post a Comment