Na Fatina Mathias, Dodoma
BENKI ya NMB imetoa msaada wa
shilingi milioni 10 kwa ajili ya skuli na hospitali katika kata ya Kibaigwa
ikiwa ni jitihada za kuwashukuru wananchi kwa kuendelea kuwaunga katika
maendeleo ya kibenki.
Hayo yalibainishwa na Meneja
Kanda ya Kati, Gabriel Ole Loibanguti,katika ufunguzi wa tawi jipya la benki
hiyo.
“Kwa kutambua nia ya kuendelea
kuchagangia huduma mbalimbali, benki ya NMB imetoa kiasi hicho cha fedha kwa
ajili kuchangia maendeleo ya wanachi wa Kibaigwa kama shukrani zetu,” alisema.
Alisema fedha zitakabidhiwa
pale uongozi wa benki hiyo utakapokaa na wa wilaya ya Kongwa.
Alisema kabla ya kufunguliwa
kwa tawi hilo, wananchi walikuwa wakifuata huduma za kibenki makao makuu ya wilaya
Kongwa na wengine kusafiri hadi Dodoma mjini.
Alisema kufunguliwa kwa tawi
hilo kunatokana na wananchi na wafanyabiashara wa soko la mahindi Kibaigwa
kuhitaji huduma hiyo kutokana na kutembea na fedha zao mkononi na hivyo kuhatarisha
maisha yao.
Aidha alisema kufunguliwa kwa
tawi hilo, NMB inafikisha jumla ya matawi ya benki hiyo kufikia 150 na zaidi ya
mashine 500 za ATM kwa nchi nzima.
Akizindua benki hiyo, Naibu
Spika na Mbunge wa Kongwa, Job Ndugai,aliishukuru benki hiyo kwa kutambua
umuhimu wa kuwapelekea wananchi huduma hiyo.
Alisema awali usalama wa fedha za wananchi na
wafanyabiashara wanaouza mazao na matrekta zilikuwa mashakani kutokana na
wezi na majambazi.
Alisema tawi hilo litawasaidia wananchi
wa eneo hilo kufaidika na mikopo inayotolewa na benki hiyo jambo ambalo
litasaidia kuinua vipato na uchumi wa
eneo hilo.
Aliiomba benki hiyo kuwapunguzia wananchi masharti ya mikopo inayotolewa kwao
pamoja na riba zinazotozwa ili kujenga uhusiano mzuri
kutoka idara hizo.
No comments:
Post a Comment