Habari za Punde

Ujenzi ‘masjid Qaboos’ kukamilika 2016

Na Hafsa Golo

Msikiti mkubwa unaojengwa na Mfalme Qaboos wa Oman ambao una uwezo wa kusaliwa na waumini zaidi ya 1,000  kwa wakati mmoja, umefikia hatua nzuri ya ujenzi wake na na unatarajiwa kukamilika mwaka 2016.

Hayo yamebainika wakati Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali, Mhe. Ali Juma Shamuhuna, alipotembelea msikiti huo kuangalia ujenzi unavyoendelea.

Meneja wa mradi wa ujenzi wa msikiti huo, Mhandisi, Ahmed Khalfan Al-shukaili, alisema  ujenzi  ulitarajiwa kukamilika mwaka ujao  lakini haitowezekana kwa sababu ya  kuchelewa baadhi ya vifaa.

Aidha alisema msikiti huo unajengwa kwa kiwango cha juu ili kuhakikisha unadumu kwa zaidi ya karne moja bila kujitokeza athari.


“Msikiti tunaojenga utapendeza kama Mfame alivyoagiza na Mwenyezi Mungu akijaalia utadumu milele bila kujotokeza hitilafu,” alisema.

Naye Waziri Shamuhuna, alisema  msikiti huo pia utakuwa na chuo cha kiislamu kitakaochukua zaidi ya wanafunzi 100 kwa wakati mmoja.

Mkuu wa Chuo cha Kiislamu Mazizini, Dk. Muhyddin Ahmad (Maalim Siasa), alisema iwapo chuo hicho kitaanzishwa wanafunzi watafundishwa na walimu wazalendo.


Alisema wapo walimu wanne wenye shahada ya uzamivu (Phd) na 21 shahada ya uzamili na kwamba walimu 18 wako masomoni nje ya nchi wakisomesha shahada ya uzamili na uzamivu. 

3 comments:

  1. Andika vizuri. Huo msikiti unajengwa wapi?

    ReplyDelete
  2. Hawa waandishi wa siku hizi ndio hivo hawaelezi yakaeleweka story hajakamilika. Msikiti unajengwa wapi ?

    ReplyDelete
  3. Huo msikiti unajengwa mazizini opposite na kituo cha polisi sawa

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.