Na Masanja Mabula, Pemba
Mtu mmoja amekutwa amekufa maji
kando ya ufukwe wa bahari kufuatia chombo chake cha kuvulia kupigwa na dhoruba kali na kisha kupinduka na
kuzama baharini.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi
mkoa wa kaskazini Pemba, Shekhan Mohammed Shekhan, tukio hilo limetokea siku ya
Alkhamis ya Januari 15 mwaka huu saa 7:00
mchana baada ya mtu huyo kutoonekana kwa muda mrefu.
Alimtaja mtu huyo kuwa ni Ali
Omar Juma (56) mkaazi wa kisiwa cha Fundo ambaye aliondoka nyumbani kwake juzi asubuhi
kuelekea baharini kwa shughuli za uvuvi
.
Alisema jeshi la polisi limechukua hatua za kitaalamu
ikiwa ni pamoja na kupeleka daktari kwa ajili ya kufanyia uchunguzi ambapo
uchunguzi wa daktari umebaini mtu huyo alikufa baada ya kunywa maji mengi.
Kufuatia tukio hilo, Kamanda
Shekhan aliwataka wananchi hususani wavuvi kuacha tabia ya kwenda bahari mmoja
mmoja bali wawe na utaratibu wa kufuatana wawili wawili ili kuweza kusaidiana
panapotokea matatizo.
Aidha aliwataka watu wanaotumia
bahari kuchukua tahadhari hasa katika kipindi hiki cha upepo.
No comments:
Post a Comment