Na Mariam Cyprian, Tanga
Mtuhumiwa Ephata Edward aliekuwa
na miripuko 475 aina ya baruti iliyokamatwa na askari waliokuwa doria mkoani Tanga,
anaendelea kuhojiwa na jeshi la polisi kuhusiana na tuhuma za kusafirisha miripuko
hiyo bila kibali.
Mtuhumiwa ambaye ni mkazi wa
jijini Arusha amekabidhiwa mikononi mwa
makashero wa polisi Januari13 siku moja baada ya miripuko hiyo kukamatwa
eneo la njia kuu ya barabara ya Kilimanjaro- Tanga- Dar es Salaam.
Miripuko hiyo ilikuwa ikisafirishwa kwa gari la abiria ikipelekwa
jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa polisi mkoa wa
Tanga,Frasser Kashai, ameliambia gazeti hili kuwa askari wake wanaendelea kumuhoji
mtuhumiwa na wakati wowote atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili
baada ya upelelezi kukamilika.
"Mtuhumiwa yupo mikononi
mwetu tunaendelea naye,tunataka kujua kwanini asafirishe miripukobila
kibali,alikuwa anaipeleka wapi na kufanya nini,kwa kuwa miripuko yenyewe ni
hatari na kibaya zaidi ilikuwa ikisafirishwa kwenye gari la
abiria,"alisema.
''Mwenye mamlaka ya kusafirisha
miripuko au kumiliki ni wale wenye machimbo ya madini kwa ajili ya kupasulia
miamba na wenye vibali maalumu huyo hatukumuelewa kwa kuwa alikuwa hana kitu
chochote cha kuufanya mzigo huo uwe halali,” alisema.
Kamanda Kashai alipiga marufuku
baadhi ya watu kumiliki miripuko ya aina hiyo bila vibali kwa kuwa ni hatari na
inaweza kutumiwa vibaya na watu wasiokuwa waadilifu kusababisha madhara.
Hili ni tukio la pili la miripuko
ya aina hiyo kukamatwa na jeshi la polisi mkoani Tanga lakini jitihada za
wananchi zinahitajika katika kutoa taarifa za watu wa namna hiyo.
No comments:
Post a Comment