Na Fatuma Kitima,DAR ES SALAAM
MSHITAKIWA Abdul Koroma kutoka
Sierra Leone ambaye alitumiwa kwa kosa la dawa ya kulevya amejaribu kutoroka
kwa kuruka uzio wa mahaka ya Kisutu jijini Dar es Salaam akiwa chini ya ulinzi
wa askari magereza na wengine.
Katika juhudi za kumdhibiti
alipata majeraha baada ya kufyatuliwa risasi.
Akizungumza jana jijini Dar es
Salaam, Kamishna polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, alisema mtuhumiwa
alikuwepo mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusomewa mashtaka yanayomkabili.
Alisema hadi sasa hawajui
kwanini alikuwa anataka kutoroka hivyo watamuhoji na kujua chanzo cha kufanya
hivyo.
Aidha aliwaonya watu
watakaofanya vurugu katika mkesha wa mwaka mpya wa 2015.
Alisema polisi wamejipanga
kikamilifu kupambana na watu watakaofanya vurugu kwa kuhakikisha sherehe hiyo
inasherekewa kwa amani na utulivu.
Alisema katika suala zima la
ulinzi jeshi la polisi litashirikiana na kampuni binafsi za ulinzi ili kufanya
kazi kwa ufanisi na kushughilikia wale wote watakaosherekea kwa fujo.
Aidha alieleza kuwa kila barabara wameweka
ulinzi ikiwemo barabara ya viwanja vya
kimataifa vya Mwalimu Nyerere.
Alianisha kuwa kuna baadhi ya
watu waliomba vibali vya kupiga baruti hata hivyo,watasimamiwa na polizi kuanzia
saa sita kamili hadi na dakika tano.
Aliongeza kuwa kwa upande wa
madereva wa magari ni marufuku kuendesha
gari huku akiwa amelewa kwani kufanya
hivyo ni kosa.
No comments:
Post a Comment