Na Joseph Ngilisho,Arusha
Uamuzi wa nchi za Jumuiya ya
Afrika Mashariki (EAC) kutumia mtandao mmoja wa simu za mkononi ifikapo Julai
2015, utasaidia kurahisisha huduma za
mawasiliano katika nchi hizo.
Hayo yalisemwa mwishoni mwa
wiki na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo, Dk. Enock Bukuku, wakati akizindua mfumo wa malipo kwa nchi za EAC kwa kutumia kadi ya Umoja iliyofanyika mjini hapa.
Alisema
hivi sasa wamekuwa wakitumia mitandao tofauti ya simu
kwa kila nchi ambapo mchakato wa
kuwepo mtandao mmoja wa simu kwa nchi hizo
utarahisisha huduma za mawasiliano.
Aliongeza
pamoja na nchi hizo kutumia mtandao
mmoja wa simu pia wataweza
kutumia kadi za Umoja kwa kupata huduma
za kibenki katika nchi zote na katika
benki ambazo zimeunganishwa na mfumo wa Umoja Switch.
Alisema
mteja yeyote mwenye kadi ya Umoja ataweza kupata huduma za kibenki kwa benki yeyote
katika nchi za EAC na kuepuka usumbufu wa kuwa na kadi nyingi.
Wakati huo huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Mitandao ya Umoja Switch,Danford Mbilinyi, alisema walianza na mabenki sita
yaliyoanza kutumia huduma hiyo ambapo
hadi sasa hivi yamefikia mabenki 27 huku wakianza na ATM za umoja 30 hadi kufikia 2000 katika nchi za EAC.
No comments:
Post a Comment