Meneja wa Baraza la Habari Tanzania MCT Ndg. Suleiman Seif Omar, akitowa mada kuhusiana na kuripoti habari za Ukimwi kwa waandishi wa habari wa Zanzibar, kuchukua tahadhari katika kuripoti habari hizo kwa usahihi na bila kuwanyanyapaa Wananchi wanaoishi na VVU, mafunzo hayo yameandaliwa na Tume ya Ukimwi Zanzibar kwa Waandishi wa habari iliofanyika katika ukumbi wa Ekrotanali Unguja.
Badhi ya Waandishi wakifuatilia hafla hiyo ya kuripoti habari za Ukimwi Zanzibar wakimsikiliza mtoa mada.iliowasilishwa na Ndg. Suleiman Seif.
Mtoa mada Suleiman Seif akionesha moja ya kijalida kinachotolewa na ZAC kuhusiana na Elimu ya Ukimwi kwa Wananchi.
Afisa wa Tume ya Ukimwi Zanzibar akitoa mada kuhusiana na Vyombo vya Habari vinasaidia nini, katika kuelimisha na kuripoti habari za Ukimwi.wakati wa mafunzo ya kufanya uchunguzi na kuripoti habari ya Ukimwi bila ya kunyanyapaa waathirika.
Waandishi wakipitia moja ya toleo la kitabu kinachozungumzia maswala ya Ukimwi.
No comments:
Post a Comment