Na Mwandishi Wetu
TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesogeza mbele tarehe ya kuanza
kuandikisha wapiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura.
Zoezi hilo lililokuwa lianze Februari 19 mwaka huu sasa litaanza
kufanyika Februari 23 katika mkoa wa Njombe.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu,
Damian Lubuva, alisema sababu ya kusogeza mbele ni kuchelewa kufika vifaa vya
kuandikisha.
Alisema vifaa vilivyopo kwa sasa ni 250 tu ambavyo vilitumika katika
uandikishaji wa majiribio na vifaa vyengine 7750, vinasubiriwa kufika nchini
hivi karubuni.
Aidha alisema sababu nyengine ya kuahirisha ni kuitikia wito wa wadau
hasa vyama vya siasa vilivyoomba zoezi hilo lisogezwe mbele ili kupata muda wa
kujiandaa.
Alisema vyama vya siasa vitatumia muda uliobakia kuwaandaa mawakala wao
kwa ajili ya kushiriki zoezi hilo.
Uandikishaji wa wapiga kura wapya utafanywa kwa kutumia Teknolojia mpya
ya Biometric Vote Regstration ( BVR).
Mfumo huo mpya ni wa kuchukua au kupima taarifa za mtu za kibaiolojia au
tabia ya mwanadamu na kuhifadhi katika kanzi data kwa ajili ya utambuzi.
No comments:
Post a Comment