Na Fatma Kassim
JESHI la Polisi kwa
kushirikiana na Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi, inawashikilia vijana wawili
waliokutwa wakibadilisha tarehe ya matumizi katika ‘body spray’ aina ya Smart, zilizomaliza muda
wake wa matumizi mwaka 2014 zinazomilikiwa na kampuni ya Izmir.
Vijana hao ni Sultan
Abdalla Okolo (29) mkaazi wa Fuoni na Siraj Maulid Mkara (29) wa Mwera ambao walikamatwa katika mtaa wa Fuoni
Maharibiko wakifanya shughuli ya kubadilisha tarehe ya matumizi ambapo jumla ya
boksi mbili tayari walikuwa
washazibadilisha muda wa matumuzi.
Mkuu wa biashara na uendeshaji
wa bodi hiyo, Abdulazizi Shaib Mohammed, alisema waliwakuta vijana hao wakiwa
na zana mbali mbali za kubadilishia muda wa matumizi wa bidhaa hizo ambapo
walikutwa wakiwa na tina, pamba, viti vya kusafishia meno, brash, rangi na
viwembe.
Alisema ‘body spray’
ambazo zilikuwa zishabadilishwa waliziandika tarehe ya kumaliza muda wa matumizi mwaka 2015 na kila boksi ilikuwa
na jumla ya chupa 60 ambazo zilikuwa zipelekwemadukani kuuzwa.
Vijana hao wana wanatarajiwa
kupelekwa katika vyombo vya sheria kuchukuliwa hatua.
No comments:
Post a Comment