MKUU wa taluma kutoka wizara ya elimu na mafunzo ya
amali Pemba, Mkubwa Ahmed Omar, akifungua mafunzo ya siku mbili kwa waalimu wa
somo la uraia kisiwani humo, yalioandaliwa na kituo cha huduma za sheria
Zanzibar ‘ZLSC’ na kufanyika ukumbi wa skuli ya maandalizi Madungu mjini Chake
chake, kulia ni Mratibu wa kituo hicho Fatma Hemed Khamis na kushoto ni afisa
mipango wake Safia Saleh Sultan, (picha
na Haji Nassor, Pemba).
MRATIBU wa kituo huduma za sheria Zanzibar
ZLSC tawi la Pemba, Fatma Hemed Khamis, akiwaonyesha waalimu wa somo la uraia
kisiwani humo, katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, wakati akitoa mada juu ya
ufafanuzi wa katiba hiyo, kwenye mafunzo yaliondaliwa na ZLSC na kufanyika
skuli ya Mandalizi Madungu, (Picha na
Haji Nassor, Pemba).
WAALIMU wa somo la uraia kisiwani Pemba wakimsikiliza
afisa mipango wa kituo cha huduma za sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Safia
Salehe Sultan (hayupo pichani), wakati akiwakaribisha waalimu hao kwenye mafunzo ya
haki za binadamu yaliondaliwa na ‘ZLSC’ na kufanyika skuli ya Mandalizi Madungu
mjini Chake chake, (Picha na Haji
Nassor, Pemba).
No comments:
Post a Comment