Na Ali Issa na Rahma Hamiss Maelezo –Zanzibar.
Wizara ya Mawasliano
na Miundombinu Zanzibar imedhamiria kununua vifaa vya upekuzi wa mizigo na
abiria katika Bandari ya Zanziabr katika mwaka ujao wa fedha.
Hayo yamesemwa
huko Baraza la Wakilishi nje ya Mji wa
Zanzibar na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Issa Haji Ussi (Gavu) wakati akijibu
suali la Mwakilishi Jaku Hashim Ayuob alietaka kujua sababu ya Serikali kushindwa
kuweka vifaa vya ukaguzi kama ilivyo katika
bandari ya Tanazania bara ili kuepusha vitendo vya uvunjifu wa haki za
binaadamu ikiwemo kuwapapasa abiria katika Sehemu zao za siri.
Amesema Wizara
yake imeamua kununua vifaa hivyo ili
kuweka usalama zaidi kwa kugundua vitu hatarishi kufuatia ongezeko kubwa la abiria na mizigo wanao ingia
na kutoka katika bandari hiyo.
Amesema
mashine hizo zitanunuliwa mwaka ujao wa fedha ambapo mradi huo tayari
umeshaingizwa katika bajeti ijayo ya Shirika la Bandari Zanzibar ili kuondoa kasoro
ziliopo za kiusalama na haki za kibinaadam.
Aidha alifahamisha
kuwa kwa sasa njia inayotumika kuwachunguza abiria na mizigo ni kuwapekuwa kwa
mikono jambo ambalo limepitwa na wakati na linapelekea abiria kukosa huduma kwa haraka.
Hata hivyo
alieleza kuwa katika upekuzi huo wanawake hupekuliwa na wanawake weziwao na
wanume hupekuliwa na wanaume weziwao kwa mpangilio maalumu.
“Kwaza
naomba kufahamisha kuwa Wizara yangu kupitia Shirika la Bandari tumeweka
utaratibu kwa wasafiri wanawake kupekuliwa na Maafisa wanawake na wanaume
kupekuliwa na maafisa wanaume wezao pale inapo bidi msafiri kupekuliwa mwilini,”
alisema Gavu.
Aidha alieleza
kwa upande wa mizigo Shirika halibagui mzigo wa mwanamke au mwaname kwani
mizigo hiyo hupekuliwa na afisa aliepo
wakati huo na ndio utaratibu wa kawaida
katika bandari zote.
Na Ali Issa
na Rahma Khamis Maelezo Zanziabr.
Shirika la
umeme Zanzibar (ZECO) linadaiwa zaidi ya
shilingi bilioni 50.8 na Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) ambazo ni malimbikizo ya madeni ya miezi ya
nyuma hadi kufikia mwezi Machi mwaka huu.
Naibu waziri wa Wizara ya Ardhi, Maji,Makazi na
Nishati Haji Mwadini Makame ameeleza hayo katika Baraza la Wawakilishi wakati akijibu swali
la Salim Abdalla Hamadi alietaka kujua kiasi cha fedha ambacho ZECO inakusanya
na inachodai kutoka kwa wateja wake na
kiasi cha fedha wanachodaiwa na TANESCO.
Amesema Shirika
la umeme la Zanzibar limekuwa likipata hasara kutokana na kupanda kwa gharama
za ununuzi wa umeme kutoka TANESCO na bei ya chini wanayowauzia wateja wao.
Alieleza
kuwa sababu nyengine ya kushindwa kulipa TANESCO ni makusanyo
kidogo kutoka Taasisi za Serikali na
Mashirika ya Umma.
Amewaeleza
wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuwa hadi kufikia mwezi Machi 2015 ZECO linawadai wateja wake zaidi ya shilingi
Bilioni 33.02.
Akitoa
ufafanuzi wa deni hilo alisema wateja wa kawaida wanadaiwa shilingi Bilioni
9.01, Taasisi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar shilingi Bilioni 22,52 na
shilingi Bilioni 1,45 wanadai Taasisi za
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Amesema hasara
hiyo imeonekana katika mahesabu ya Shirika hilo ya mwaka ulioishia tarehe 30
juni 2014.
Ameongeza kusema
kuwa pamoja na madeni na hasara wanayoipata Shirika limeweza kutekeleza
majukumu yake ya msingi ikiwemo kupeleka umeme vijijini.
“ZECO limeweza
kujiendesha pamoja na kupata hasara kwani
imeweza kulipa robo tatu ya ankara yake
kwa TANESCO na robo inayobakia hutumia kwa shughuli zake za kawaida,” alieleza
Naibu Waziri.
Alisema
katika kuhakikisha ZECO inapunguza deni
hilo wamekubaliana na TANESCO kulipa ada ya mwezi na kutoa shilingi Bilioni moja kila mwezi.
Aidha alisema
ZECO imeweza kulipa ada kwa miezi minne na
kulipa ziada ya milioni 500 kwa TANESCO
IMETOLEWA NA
HABARI MAELEZO ZANZIBAR
No comments:
Post a Comment