Habari za Punde

Mhe Membe Atangaza Nia na Kusema Watanzania Wanahitaji Seikali Itakayo Simamia Utawala Bora Haki na Uadilifu.

Na Mwandishi Wetu Lindi.

MJUMBE wa Kamati kuu ya CCM na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Kamillius Membe, amesema Watanzania wanahitaji serikali itakayosimamia Utawala Bora, haki na Uadilifu, yenye kujali jinsia na kuzingatia dhima ya uwajibikaji.

Amesema ili kufikia azma hiyo ni jukumu la Chama cha Mapinduzi kuweka miiko ya viongozi ili kuzuia mianya ya rushwa na kusiisitiza haja ya kuwepo uadilifu miongoni mwa viongozi.

Membe amesema hayo leo katika  viunga vya CCM Mkoa wa Lindi, wakati alipotangaza nia ya kugombea kiti cha Urais wa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi.

Akizungumzia vipaumbele vyake iwapo Chama chake kutamteua kugombea nafasi hiyo na kufanikiwa kuwa Rais, Membe alisema kuna haja kwa badhi ya sheria ikiwemo ile ya kuzuia rushwa kurekebishwa.

Alisema Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la rushwa ambapo baadhi watu wakiwemo viongozi, kujikita katika kupokea rushwa na kufanya ufisadi, jambo linaloharibu sifa ya nchi.


Alisema iwapo atachaguliwa kuiongoza Tanzania, suala la Ulinzi n Usalama ni miongoni mwa mambo makuu yatakayoshughulikiwa na kuonya kuwa hatakuwa na kigugumizi dhidi ya wahalifu wanaohusika katika mauaji ya Albino,Madawa ya kulevya,ujambazi na ugaidi.

Alisema atasimamaia kwa nguvu zote kulinda mipaka ya Tanzaniaili kuwahakikishia maisha salama wananchi pamoja na kuimarisha vyombo vya Usalama ikiwemo Polisi kwa kuvipatia vifaa muhimu vya kisasa vyenye uwezo wa kuwakamata wahalifu.

Aidha alisema ataaendeleza Tunuya taifa kwa  kuhkikisha Muuungano wa Tanzania unadumu na kuainisha kuwa hatakuwa tayari  kumvumilia yeyote atakaejaribu kuhatarisha muuungano huo.

Alisema kuna baadhi  ya Wazanibari wanakebehi Mapinduzi  matukufu ya Zanzibar ya 1964, hivyo  kuahidi kuwashughulikia, sambamba na kufanya juhudi za kujenga mazingira bora katika kuimarisha uchumi na maendeleo ya  nchi hiyo.

Akigusia juu ya uimarishaji wa uchumi, Membe alisema atasimamia uanzishaji wa viwanda vidogo vidogo pamoja na kuyapa uwezo  makampuni binafsi ili hatimae yaweze kutoa jaira kwa vijana.

Alifafanua kuwa Serikali yake itajenga vituo vya ufundi na  VETA ili vijana waweze kupata maarifa na ufundi katika masuala mbali mbali na hatimae kuweza kujiajiri.

Katika hatua nyingine Membe alisema suala la usawa wa kijinsia nalo litapewa kipaumbele, kwa lengo la kuondoa dhuluma na udhalilishaji  dhidi ya akinamama.

Alisema pia Serikali itanzisha mabenki maalum kwa ajili ya wanawake ili waweze kujiendeleza kiuchumi na kijamii.

Mapema Waziri huyo alisema ameamua kujitosa katika kinyanganyiro hicho baada ya kujiridhisha kuwa ana sifa zote 13 zilizohitajika kwa wagombea.

Alisema amekuwa mtumishi mwenye mafanikio makubwa ndani na nje ya chama chake na kufanikiwa kushika nyadhifa mbali mbali ikiwemo za Uwaziri.

Alieleza kuwa anakusudia kuendeleza umoja na mshikamano  miongoni mwa Watanzania kama ilivyoaisiswa na hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Nae mmoja wa Mawaziri katika Baraza la kwanza la Mawaziri, Sir George Kahama alimsifia Waziri Membe na kusema ni mtumishi msafi, mwenye kuchukia rushwa na ufisadi, ambae katikadi chote cha utumishi wake alijitolea kuwatumikia Watanzania.

Alisema kiongozi huyo ni mtaalamu katika masuala a usalama na kuanisha kuwa hilo ni jambo muhimu katika  ustawi wa taifa.


Hatua ya Waziri Membe kutangaza nia ya kugombea kiti cha Urais kupitia CCM, inakifanya chama hicho ,kufikisha idadi ya wagombea 22 tangu mchakato huo kuanza

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.