Habari za Punde

Wachimba mawe Vitongoji: Tunauza roho zetu kusaka rizki


 Na Zainab Atupae, PEMBA

“Tunauza roho zetu  kwa kusaka riziki…. mikono iende kinywani na midomo iweze kucheza cheza ‘’.

Hayo ni maneno ya wachimbaji wa mawe eneo la Kwareni  Vitongoji ndani ya wilaya ya Chakechake .

“Hatuna hila wala uwezo  wakutafuta  kazinyengine  zakutuwezesha maisha yetu  ambayo hatuna ajira’’ walikua wanalalamika nilipofika machimboni.

 Pamoja na yote hayo kazi hii  ya uchimbaji wamawe  ni hatari wakati mwengine  kupoteza viungo na  kupoteza maisha pia.

 “Najitahidi tu lakini mawazo telee  kichwani na machozi kunilegalega  nikikumbuka mwenzangu  Hamadi Zahor  Faki, alivyo weza kukatikiwa na mwamba wa jiwe na kufariki hapo hapo” alinieleza kwa uchungu Abdalla ‘bati ambae nikiongozi wa chimbo hilo.

 Hao ni  baadhi tu ya mamia ya watu, wakati wanapokuwa wakiendelea na kazi yao ya  uchimbaji wa  mawe katika eneo hilo kisiwani Pemba , wanapo pambana  na kazi ngumu na yenye kuhitaji ujasiri.

 Wengine huchimba mawe hayo hata kwa kutumia mapango, na kujikata vidole, huku nyundo nazo zikitawala eneo hilo kwa Kware, ambao palichangamka ni sawa na soko la Mwanakwerekwe Unguja.

Kubwa ambalo unaweza kulishangaa na kudondokwa na machozi hasa kwa alie na huruma, ni kuona wapo wanachimba na kuvunja mawe wakikosa zanabora za kufanyia kazi  sambamba na mbinu bora za  kuchimbia mawe .

Kalamu ya makala hii, haikutosheka na jicho la mbali, ndipo ilipojongea karibu na kumsaka alau mmoja,  na kumkatisha kazi ili aweze kuzungumza name.


“Kaka habari…..naam unataka mawe au wewe ni afisa kutoka Idara ya mazingira…hapana nahitaji kuzugumza na wewe..hapo alikuwa kijana mmoja akiwa ameroa jasho.

Kw aliavyokuja haamini kwamba sitonunu mawe, licha ya kunipokea vyema na hasa baada ya kujua alitembelewa na mwandishi wa habari.

Yeye nilimtoa akiwa chini  ya mwamba  mkubwa wenye ugumu  ambapo mimi nilisita na  kidogo  kwenda huko,  lakini kupiga moyo konde niliamuwa  kuvua viatu  vyangu   vyenye gundi  ambavyo  nilizowea kuvivaa  kwenda kwenye sehemu kama hizi zenye mwamba.

‘’ Tukiwa katika  kazi hiyi ya uchimbaji  wa mawe  na kuyakata miamba ya mawe na kuilinda miamba hiyo kwa kuweka kifusi kwaajili ya kulinda mporomoko wa aridhi unaweza ukatokea,’’ walisema wachimbaji hayo.

Mchimbaji huyo, alinieleza kwamba, miamba ya mawe ndio inayo zuwiya mmongonyoko wa ardhi  lakini wakati wanapo endelea  kuchimba, baadae huchukuwa fusi  linalokatiwa  mawe hayo na kulimwaga .

Abdalah Mohamed  [ Bati] ambae ndie kiongozi  wa kware hiyo  ya  mawe, yeye binafsi  alisema  ajira kwao ni tatizo kubwa, lakini wameweza kujiajiri na kuweza kupata maendeleo.

Alisema  wachimbaji mwanzo ulikuwa hauna mapato kutokana na mauzo yalikuwa yakianzia shilingi  5000 kwa gari moja  na hadi  sasa  ni shilingi 35,000.

Bati alinifahamisha kuwa licha ya kazi ngumu ya kulitoa jiwe chini ya mwamba hadi juu, kwa ajili ya kuliuza, bado bei ni ndogo, ingawa wanatarajia kuongeza shilingi 5000 na kufikia shilingi 40,000 kwa shehena moja ya gari.

 ‘’Maisha ni kitenda wiwi……lazima utafute njia ya kikiteguwa na  kukipatia ufumbuzi ilikuweza kupata  njia ya kupita na weza kuona mwanga ulio finikia usoni.’’,alisema  Abdalah  bati.

Kuhusu ukosefu vietendea kazi vya kutosha vya kuchimbia mawe  ambavyo ndio chanzo kiubwa cha kutafutia maisha  alisema, ni kikwazo kikubwa kwao.

“Tunachimbia kwa kutumia sururu, vipanga, majembe  kwa ajili ya kutolea vifusi na tindo  kwaajili ya kutolea mawe, yote hayo nguvu ndio jambo la mwanzo’’,alifafanua Bati.

Kwa sasa wanahitaji vifaa vya kisasa ambavyo wanaamini kama wakipatiwa ndio watafanyaka kazi zao kwa ufanisi, ambapo hapo ndio serikali nayo iwape nguvu.

Lakini vipi kuhusu uharibufu wa mazingira  katika suala kukata miamba  yamawe, nilimuuliza sualini hili bati, naye  alisema wameweza kujiaandaa vizuru kwa kupambana  kwa kuweka fusi kila sehemu wanayo  kata mawe.

‘’Mbona sisi wenyewe tuwakua wakali kwamba eti umeshafukua shimo na kutoa mawe kisha uliwache, tunakukamata hadi ufukie’’,alisema akimaanisha ameshapata taaluma japo kidogo.

Othuman Khamis naye ni mchimbaji katika kware hiyo, yeye analalamikia kutokuwa na barabara ya uhakika kutoka afisini kwao hadi njia kuu.

‘’Inawezekana serikali haioni mchango wetu na ndio maana tumekuwa tukipiga kelele kuhusu ujenzi wa barabara kwa muda mrefu bila ya mafanikio’’,alilalamika.

Kwao barabara ni tatizo sugu hasa siku za mvua, ambapo hukosa wateja na wanokuja hununua kwa bei ya chini, maana bado barabara ni ya udongo.

 Lakini wachimbaji hawa wakaziomba taasisi husika kuwaongeza elimu ya uchimbaji mawe ili wafanye kazi zao kwa ufanisi.

Wamekuwa wakifanya kazi hiyo kwa mazoea jambo ambalo wakati mwengine hujihisi kutengwa na asasi za kiraia na hata serikali kuu, kwa vile hukosa hata kutembelewa na viongozi na kuwapa maelezao.

Lakini sheha wa shehia ya Vitongoji ambako kware hiyo ndio iliko Salim Ayoub, aliwataka wachimbaji hao kwanza wao kujikusanya pamoja.

‘’Njia kubwa ya wao kujikwamua na umaskini na hata kupata elimu waitakayo wahakikisha wanakuwa na ushirika wao ambao sauti zao zinaweza kufika mbali zaidi’’,alifafanua sheha.

Said Khatibu yeye ndie mkuu wa kware hiyo, yeye alisema sio busara eneo wanalochimba wachimbaji hao kupelekewa gari la kuchimbia kwani huwapa hofu vijana hao.

  Alisema kuwepo kwa   sehemu hiyo ni muhimu kwa  kwananchi kwa ujumla kwa kuwapatia kazi mzuri na kuwaingizia mapato kwa ujumla.

 Asilimia kubwa ya wananchi wa Vitongoji  wako huko kware ya binafsi yamawe   kwakazi ya uchimbaji wa  mawe , ambayo ndio ajira yao.

 Wakaazi hawa shehia za Vitongoji na wengine hata kutoka Uwandani, wanaona wakati umefika kwa serikali kuthamini juhudi zao za kujipatia mapato.


Ama kweli mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe, haya huwezo kuyashuhudia popote kama sio kware ya Vitongoji Wilaya ya Chakechake mkoa wa kusini Pemba.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.