Habari za Punde

Madaktari Diaspora Wakiondoka Zanzibar baada ya Kumaliza Zoezi la Kutoa Huduma ya Saratani ya Matiti, Kisukari na Meno.

Madaktari Diaspora Washinton wakiwa katika bandari ya Zanzibar wakijiandaa kurudi nyumbani baada ya kumaliza ratiba yao Tanzania ya kutoa hudua ya Afya kwa Wananchi wa sehemu hizo mbili wakiwa Tanzania wameletwa na Jumuiya ya Watanzania Washington wakiongozana na Rais wa Jumuiya hiyo Ndg Iddi Sandaly na Mjumbe wa Kamati Bi Asha Nyanganyi. Zanzibar walikuwa wageni swa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora Zanzibar na Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ).
Madaktari haio wakiwa katika bandari ya Zanzibar wakijiandaa kurudi nyumbani kwa boti ya Kampuni ya Azam Marine Kilinanjaro v. 
Wakiwa katika chumba cha VIP katiba bandari ya Malindi Zanzibar wakisubiri taratibu za usafiri bandari hapo ili kurejea nyumbani.
       Mjumbe wa Kamati ya Jumuiya ya Watanzania Washington Asha Nyanganyi akiwa na ujumbe huo.
                   Wakiwa katika chumba maalum cha VIP  katika bandarini malindi Zanzibar.

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora Zanmzibar Ndg Adila Hilal Vuai Rais wa Jumuiya ya Watanzania Washington Ndg Iddi Sandaly na Afisi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Diaspora Zanzibar Ndg Salum Ramia wakibadilishama mawazo katika ukumbi wa VIP bandari kupongezana kufanikisha ziara hii muhimu kwa Wananchi wa Zanzibar kupata tiba na ushgauri nasaha juu ya magonjwa ya Meno, Saratani ya Matiti na Kisukari.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.