Habari za Punde

Mhe.Majaliwa Ameagiza Usimamiaji na Udhibiti wa Ubora wa Elimu

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza kwenye  maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro(MUM), alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro Juni 20, 2025. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

 ▪️Asema lengo ni kuendelea kutoa wahitimu wenye uwezo wa kukidhi vigezo vya kimataifa

 

▪️Rais Dkt. Samia atoa milioni 100 kuchangia maendeleo ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameitaka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na TAMISEMI pamoja kusimamia na kudhibiti ubora wa elimu inayotolewa kuanzia elimu ya msingi mpaka elimu ya juu ili kuendelea kukidhi viwango vya kitaifa, kikanda na kimataifa.

 

Ametoa maagizo hayo leo (Ijumaa Juni 20, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho ya miaka 20 ya Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM), kwenye viwanja vya chuo hicho mkoani Morogoro.

 

“Mamlaka zetu ziendelee kusimamia hilo kwa kufanya hivyo sio tu kutaendelea kukuza ubora wa elimu yetu, bali pia kutawawezesha wasomi nchini kukidhi viwango na mahitaji ya soko la ajira”

 

Kadhalika, Mheshimiwa Majaliwa amezitaka Taasisi za Elimu nchini ziimarishe mahusiano na vyuo vyote nchini vinavyotoa maarifa kwa vijana wa kitanzania pamoja na kuzalisha wakufunzi ili kuwa sehemu ya mtandao wa utoaji maarifa na taalum hapa nchini.

 

Aidha, Mheshimiwa Majaliwa kuwa katika kuunga mkono jitihada za wadau mbalimbali katika kuchangia maendeleo ya chuo hicho kupitia mfumo maalum wa (MUM Community Fund), Rais Dkt. Samia ametoa kiasi cha Shilingi milioni 100 ili kiendelee kutoa huduma kwa watoto wa Kitanzania

 

Mheshimwa Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa Mfumo wa Takwimu wa Sekta ya Elimu utakaowezesha upatikanaji wa takwimu zote za sekta hiyo ambao utakuwa na uwezo wa kupokea takwimu mbalimbali zinazohusiana na elimu kutoka katika mifumo mingine ya Serikali ikiwemo NIDA, RITA na Wizara ya Mambo ya Nje.

 

Kwa Upande wake Naibu Waziri wa Elimu Qs Omar Kipanga amesema kuwa katika kipindi cha miaka 20, chuo hicho kimefanikiwa kuwa na progrma zaidi ya 32 kutoka program mbili wakati kinaanza na kimefanikiwa kutoa wahitimu zaidi ya 15,000.

 

“Wahitimu hawa wamekuwa wwamekuwa wa kupigiwa mfano katika kazi na maadili inayofanya waaminiwe katika nafasi mbalimbali kwenye jamii na Serikali kaa ujumla”

 

Kadhalika, ameongeza kuwa Chuo hicho kimeweka mipango inayozingatia dira ya maendeleo ya Taifa ya 2050 na mwelekeo mpya wa Elimu Nchini Tanzania unaolenga kutoa Elimu Ujuzi, Stadi na Maarifa kwa ajili ya kuwajengea wahitimu uwezo na sifa za kujiajiri na

kuajirika katika soko shindani la ajira duniani.

 

Naye Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Dkt. Abubakar Zubeir bin in Ali ametoa wito kwa Waislam na Watanzania kwa ujumla kuweka mikakati ya kukisaidia chuo ili kiendelee kufanya vizuri na kutoa elimu kwa watanzania nchini.

 

“Waislam na watanzania tukisaidie chuo hichi, hakuna uislam bila ualimu, uislam ulipokuja ulipiga sana vita ujinga, tuwaunge mkono viongozi wetu kwa kukisaidia chuo hiki”

 

Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof Juma Assad amesema kuwa moja ya changamoto kubwa katika chuo hicho ni kukosekana kwa hosteli za wanafunzi wa kike “Namna tunavyoingeza udahili ndivyo tunavyoibua changamoto nyingine, tunataka watoto wetu wa kike wote wake ndani ya chuo”   

 

(Mwisho)

 

IMETOLEWA NA:

OFISI YA WAZIRI MKUU,

S. L. P. 980,

41193 – DODOMA.

IJUMAA, JUNI 20, 2025.


No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.