Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha leo,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala alipofika kujitambulisha Ikulu Mjini Zanzibar leo,[Picha na Ikulu.]
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akifuatana na Balozi mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Nchini Zimbabwe Lt.Gen.Mstaafu Charles Makakala baada ya mazungumzo yao leo alipofika Ikulu Mjini Zanzibar kujitambulisha ,[Picha na Ikulu.]
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Zanzibar 21.08.2015

RAIS wa
Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema
kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kuimarisha uchumi wa kidiplomasia kati ya Zimbabwe
na Tanzania hasa ikizingatiwa kuwa nchi hizo zina uhusiano wa kihistoria.
Dk. Shein
aliyasema hayo leo, huko Ikulu mjini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na
Balozi Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbabwe Mhe. Luteni
Jenerali Mstaafu Charles Laurence
Makakala, ambaye alifika Ikulu kwa ajili ya kuaga na kupata baraka za Rais.
Katika mazungumzo
hayo, Dk. Shein alimueleza Balozi Makakala kuwa tayari Tanzania na Zimbabwe zimekuwa na
uhusiano wa kindugu na wa kihistoria hivyo mkakati zaidi unahitajika katika
kuimarisha uchumi wa kidiplomasia kati ya nchi hizo ili zizidi kupata mafanikio.
Dk. Shein alisema
kuwa katika hatua za kuimarisha sekta za maendeleo sambamba na kukuza mashirikiano
kati ya Tanzania na Zimbabwe uimarishwaji wa sekta ya uchumi ina umuhimu wa
pekee hivi sasa hasa ikizingatiwa mafanikio yaliopatikana katika nchi mbili
hizo
.
Alisema kuwa
uimarishwaji wa mashirikiano katika sekta ya biashara nayo yanahitajika kwa
kiasi kikubwa kati ya nchi mbili hizo kutokana na kuwa mazuri tokea siku za
nyuma.
Aidha, alisema kuwa uhusiano na ushirikiano katika sekta ya
utalii nalo ni jambo muhimu hasa ikizingatiwa kuwa nchi ya Zimbabwe imekuwa ni
miongoni mwa nchi za Kusini mwa Bara la Afrika ambayo imekuwa ikipata watalii
kutokana na kivutio chake kikubwa cha maporomoko ya maji Victoria ‘ Victoria
waterfalls’.
Dk. Shein alisema
kuwa sekta hiyo ya utalii pia, ni sehemu ya uimarishaji wa uchumi wa
Kidiplomasia hasa ikizingatiwa kuwa Tanzania nayo ina vivutio vingi vya kitalii
vikiwemo vivutio vilivyopo katika visiwa vya Zanzibar na maeneo mengine
yakiwemo mbuga za wanyama.
Alisema kuwa ipo
haja ya kuendelea kuimarishwa uhusiano kati ya nchi mbili hizo kwa kuwepo
programu maalum za ubadilishanaji wa utaalamu na wataalamu kati ya vyuo vya
Tanzania na Zimbabwe ambapo hapo awali ulikuwepo kupitia Chuo Kikuu cha
Dar-es-Salaa na vyuo vya Zimbabwe.
Hivyo, Dk. Shein
alitumia fursa hiyo kusisitiza haja ya vyuo
vikuu vya Zimbabwe kuimarisha uhusiano na vyuo vikuu vya Zanzibar kikiwemo Chuo
Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) hasa ikizingatiwa kuwa chuo hicho tayari
kimeshaanza kusomesha Shahada ya Uzamifu ‘PhD’ katika lugha ya kiswahili.
Alisema kuwa
kutokana na hatua kubwa iliyofikiwa hivi sasa katika kuikuza lugha ya Kiswahili
kwa nchi za Afrika, lugha hiyo ni moja kati ya lugha rasmin za Umoja wa Afrika
(AU) inayozungumzwa katika mikutano yake.
Hivyo, Dk. Shein
alisema kuwa, ipo haja kwa Zimbwabwe
kuitumia fursa hiyo kuleta vijana wake kuja kujivunza lugha ya Kiswahili hapa
Zanzibar kwani pia, wapo baadhi ya wananchi wa Zimbabwe wanaozungumza
Kiswahili.
Pamoja na hayo,
Dk. Shein alisisitiza haja ya kuwepo kwa mashirikiano kwa Taasisi za utafiti wa
mazao ya kilimo kati ya nchi mbili hizo kutokana na mafanikio yaliopatikana
sambamba na mikakati iliyowekwa katika kuikuza sekta hiyo katika nchi hizo.
Sambamba na hayo,
Dk. Shein aligusia umuhimu wa kuendeleza suala zima la Diaspora kwa kuwaunganisha
na kuwaweka pamoja Watanzania wanaoishi nchini humo na kuwaeleza fursa zilizopo
nchini mwao, ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza kuekeza nyumbani.
Nae Balozi Mteule
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Zimbwabwe Mhe. Luteni Jenerali Mstaafu Charles Laurence
Makakala alitoa shukurani zake kwa uteuzi huo alioupata na kumuahidi Dk. Shein
kuwa atazidi kujenga uhusiano na kuimarisha ushirikiano uliopo kati ya Tanzania
na Zimbabwe ambao una historia tokea wakati wa kudai uhuru.
Balozi Makakala
alitumia fursa hiyo kueleza umuhimu wa kuendeleza uhusiano na ushirikiano kati
ya nchi mbili hizo kati nyanja mbali mbali za kimaendeleo hasa katika uchumi wa
Kidiplomasia ambao unaweza kuleta mafanikio kwa pande zote mbili.
Aidha, Balozi
huyo alieleza kuwa Zimbabwe kuna vitu vingi ambavyo Tanzania inaweza ikajifunza
na hatimae kuleta mafanikio hivyo, atatumia fursa hiyo kuhakikisha mafanikio
yanapatikana sambamba na kuhakikisha uhusiano na ushirikiano uliopo unaimarika.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024
2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment