Katibu wa CCM Wilaya ya Mjini Fatma Shomari akitaja matokeo
ya Jimbo la Kwahani kukamilisha majimbo ya Uchaguzi katika Wilaya yake
kukamilika kufanya uchaguzi wa Kura za maoni
baada ya kutoa matokeo ya Majimbo ya Rahaleo, Jangombe na Malindi
kubakia Jimbo hilo la Kwahani kutopata matokeo yake wakati wa kutaja majimbo
hayo.
Jimbo la Kwahani kwa Wabunge.tovyo
Kwa nafasi ya Mbunge waliojitokeza kugombea nafasi hiyo ni
Wanachama Wawili nao ni aliyekuwa Mbunge wa Zamani Mhe Hussein Ali Hassan Mwinyi na Ndg Jaffar Khamis Ramadhani ndio
waliojitokeza katika nafasi hiyo.
Kwa nafasi ya Ubunge mshindi ni Mhe Hussein Ali Hassan
Mwinyi kwa kupata kura 3098 kwa kumshinda mpizani wake Jaffar Khamis Ramadhani
kwa kupata kura 98.
Kwa Upande wa nafasi ya Uwakilishi Wanachama wa CCM
waliojitokeza kugombea nafasi hiwa walikuwa 7.
Mshindi wa nafasi ya kwanza aliyekuwa Mwakilishi wa Zamani
wa Jimbo hilo Mhe. Ali Salum Haji.
Nafasi ya Pili katika kura hizo za maoni imechukuliwa na Ndg Nassor
Shaban Ameir kwa kupata kura 671.
Nafasi ya Tatu imechukuliwa na Ndg. Machano
Mwadin Omar kwa kupata kura 642, Kwa
Nafasi ya Nne imeshikwa n a Ndg Mmaka
Hamad Hilika kwa kupata kura 508,
Nafasi ya Tano imeshikwa na Ndg Abdalla
Mohammed Abdalla kwa kupata kura 165.
Nafasi ya Sita imechukuliwa na Ndg Ameir
Juma Othman kwa kupata kura 99,na
Nafasi
ya Saba imeshikwa na Ndg Hassan Ibrahim Suleiman kwa kura 92.
No comments:
Post a Comment