Habari za Punde

Mkutano wa wazi wa msaada wa kisheria wafanyika Mtambile

 SHEHA wa shehia ya Mtambile wilaya ya Mkoani Pemba, Rajab Zaid Risasi, akizungumza kwenye mkutano wa wazi juu ya kutoa msaada wa kisheria, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, kulia ni Afisa Mipango wa kituo hicho Siti Habib Salum, akifuatiwa na Mratibu wake Fatma Khamis Hemed, mwanasheria kutoka afisi ya Mkurugenzi wa mashitaka Seif Mohamed Khamis na hakimu wa mahakama ya ardhi Salum Hassan Bakar, (Picha na Haji Nassor, Pemba)
 HAKIMU wa mahakama ya ardhi mkoa wa kusini Pemba Salum Hassan Bakari, akimpa masaada wa kisheria mwananchi mmoja wa shehia ya Mtambile wilaya ya Mkoani, wakati watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, walipofika hapo kutoa masaada wa kisheria bila ya malipo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 WANANCHI wa shehia ya Mtambile wilaya ya Mkoani Pemba, waliohudhuria kwenye mkutano wa wazi wa kutoa msaada wa kisheria bila ya malipo, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
AFISA Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC Khalfan Amour Mohamed, akigawa majarida kwa wananchi wa shehia ya Mtambile wilaya ya mkoani Pemba, yaliochapishwa na ZLSC, wakati wa mkutano wa wazi wa kutoa msaada wa kisheria, (Picha na Haji Nassor, Pemba)  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.