Habari za Punde

Nyumba yateketea na kuua watu tisa Buguruni kwa Malapa

Nyumba hii imeungua juzi usiku, mwenye nyumba amepoteza mke, watoto wanne, mama mkwe na wageni watatu walikuja kumtembelea, Jumla watu 9



10984474_1301905196490562_5658746228997238516_n
Moto ulianza kuwaka saa 9 vijana wawili wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka 16 Aisha na Ahmed walisimama Mlangoni kuomba Msaada walifungua mlango mbao ukabaki wa Grill ambao walishindwa kuufungua majirani akiwemo Salama Ally Mjumbe wa Malapa wakawaaambia Aisha na Ahmed leteni funguo Aisha na Ahmed wakaleta funguo lakini majirani wakashindwa kufungua kwani geti la Grill lilikua limeshika moto.

Baaada ya jitahidi za kuokoa na kujiokoa kushindikana ndipo watu wote tisa waliopo ndani wakaamua kukaaa chumbani kwa Bibi yao anaeitwa Bim Mdogo na Bim Mdogo akawakumbatia na huo ndo ukawa Mwisho wa uhai wao.

Waliofariki ni


Samira - Mama mwenye nyumba
Aisha - Mtoto
Ahmed - Mtoto
Abdallah
Ashraph
Bim Mdogo - Bibi
Wadh ha na mwanae walikuja kutembea akiwa na mfanyakazi wake wa kike.

3 comments:

  1. Mbona hamjaandika wazima moto wamearifiwa usiku wakati moto unateketeza, na fire station haiko mbali na hapo sehemu, lkn wamekuja asubuhi, ati kutizama chanzo cha moto nini?

    ReplyDelete
  2. Mambo kama haya, ukipiga simu fire hawaji kwa time , ukipiga simu polisi kuna majambazi hawaji kwa time, kila la emergency hamna nchi hii , mambo kama haya hutufanya wengi kutokupiga kura, maana yoyote anochaguliwa haleti faida yoyote hususan kwenye mambo kama haya lazima

    ReplyDelete
  3. Innalillahi wainna ilaihi rajiun.Alla awasameh makosa yao.na awape subra wafiwa.{Ammin

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.