STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
Pemba
15.9.2015

Makamu
Mwenyekiti wa CCM Zanzibar na Rais wa Zanzibar
na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein amesema kuwa katika uongozi wake ametekeleza
Ilani ya uchaguzi ya CCM kwa vitendo huku pia, akitekeleza vizuri uongozi wake
katika Serikali yenye muundo wa Umoja wa Kitaifa kwa amani na utulivu.
Dk. Shein ambaye ni Mgombea nafasi ya Urais wa
Zanzibar kwa tiketi ya CCM aliyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa kwenye
mkutano wa Kampeni wa chama hicho uliofanyika huko katika viwanja vya Gombani
ya Kale, Chake Chake Pemba.
Dk. Shein aliwaeleza maelfu ya wananchi
waliohudhuria mkutano huo kuwa endapo atachaguliwa tena ataendelea kuimarisha utulivu,
amani na kuendelea kuwahudumia wananchi wa Zanzibar bila ya ubaguzi wa aina yeyote
iwe wa kidini, rangi, kabila na hata mahala kwani hayo ndio maelekezo ya chama
chake.
Alitaja baadhi ya mafanikio ya uongozi wake kuwa ni
pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha ukuaji wa uchumi kutoka asilimia 4.5 hadi 7.2 ambapo kwa upande wa pato la taifa limeongezeka
hadi trilioni 1.508 kutoka trioni 2.138.
Kuhusu mfumuko wa bei kiwango alisema kitaendelea
kushuka ikiwa ni uthibitisho wa kutengemaa kwa uchumi wa taifa huku akieleza
mipango uendelezaji wa maeneo huru ya Kiuchumi ya Fumba kwa kujengwa mji mpya
pamoja na viwanda.
Kupambana na umasikini, kituo cha kulelea
wajasiriamali ambacho ni kikiubwa katika Afrika Mashariki, ni lazima kuweko na
programu maalum na hakuna njia ya mkato kama inavyoelezwa na Wapoinzani.
Aidha,
Dk. Shein alieleza mafanikio yaliopatikana katika sekta ya kilimo na kueleza
azma yake ya kuendeleza sekta hiyo huku akisisitiza kuendelea kutoa ruzuku na
kuendelea kuwasaidia wakulima.
Kwa
upande wa karafuu, alisema kuwa uwamuzi wa kuinua zao la Karafuu ni utekelezaji
wa Ilani ya CCM na kwamba hatua zilizochukuliwa la kutolibinafsisha biashara ya
zao hilo sambamba na kupandisha bei ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati wa
kuimarisha zao hilo nchini.
Dk. Shein
alibainisha kuwa uamuzi huo ulifanywa nan yeye mwenyewe na kupewa baraka na Baraza
la Mapinduzi na kumtuma Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko kutanganza uamuzi
huo.
Alisema
kuwa asilimia 80 ya bei ya karafuu duniani wamepewa wakulima huku akieleza kuwa
uongozi ni kazi na zaidi ni kuonesha njia.
Hadi sasa
alieleza jumla ya tani za karafuu 5340 zimeuzwa na kukomesha magendo ya zao
hilo kwa kuhakikisha kuwa taratibu zinafuatwa katika kuuza karafuu na hatua
inayochukuliwa hivi sasa ni kuzifanya karafuu za Zanzibar kuwa alama maalum'branding'.
Katika sekta ya barabara Dk. Shein alieleza mafanikio yaliofikiwa
kisiwani Pemba na hakuna barabara hata moja inayoungana na barabara kuu za
Pemba ambayo haina lami na zilizobaki zinatarajiwa kumaliza karibuni.
Katika kuimarisha miundombinu ya usafiri wa baharini alieleza kuwa bandari
mpya ya Mpigaduri itakayokuwa na uwezo wa kushughulikia kotena 200,000 kwa kwa mwaka
itaanza kujengwa mara baada ya kukamilika kwa jengo la uwanja wa ndege.
Aidha aliongeza kuwa Bandari ya
Wete itajengwa upya na kuwaomba wananchi wawe wastahamilivu.
Kwa upande wa wafanyakazi wa Serikali aliwaahidi kuendelea kuiamarisha
maslahi yao kama alivyofanya katika kipindi chake cha uongozi kinachomalizika
huku aliahidi endapo atachaguliwa tena atapandisha kima cha chini cha mshahara
hadi 300,000 kwa mwezi.
kuhusu utekelezaji wa Ilani ya CCM alisema
utekelezaji umefanyika kwa asilimi 90 ambapo asilimia iliyobaki itaenaendelea
kutekelezwa huku akieleza jinsi juhudi zilivyochukuliwa.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali
Idd nae alipata nafasi na kusikitishwa na maneno ya uongo yanazotolewa na kiongozi
wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad.
Balozi Seif alisema kuwa Dk. Shein amefuata Ilani
ya CCM kwa kuongeza bei ya karafuu pamoja na kuongeza idadi ya miche ya
mikarafuu sambamba na kuliimarisha zao hilo.
Alisema kuwa chama cha CUF hakina uzoefu wa
kuendesha Serikali na kueleza kuwa Maalim atakuwa mtu maarufu kwa kugombania
mara sita urais wa Zanzibar huku akieleza kuwa mwisho wa chama chake ni 2015
kwani chama hicho na yeye mwenyewe hawatoweza kufikia mwaka 2020. "2015
CUF itakufa kifo cha mende miguu juu",alisema Balozi Sif.
Aliwata Wana CCM kuendelea kushikamana na kuwa
wamoja kwa lengo la kupata ushindi wa uhakika
huku akisisitiza kuwa CCM ikishinda na Maalim Seif akikataa matokeo Dk.
Shein ataunda Serikali ya CCM pekee.
Nae Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Vuai Ali
Vuai, alisema kuwa wananchi wa Pemba mwaka huu wamedhamiria na wataleta
mabadiliko makubwa.
Alieleza kusikitishwa na tabia za viongozi wa CUF
za kuwatuma watoto pamoja na vijana kuchana picha za wagombea wa CCM
zilizobandikwa huku akivitaka vyama vyote kufanya siasa za kistaarabu.
Nao viongozi wa CCM walipata fursa ya kusalimiana
na wananchi pamoja na WanaCCM waliohudhuria katika mkutano huo na kuwapongeza
wananchi wa Pemba kwa kuonesha azma ya kukiunga mkono chama hicho.
Mohamed Aboud nae alieleza kuwa chama cha CUF
kimemuweka rehani Makamu Mwenyekiti wao
Juma Duni kwa kujiunga na CHADEMA na kusisitiza kuwa hatua hiyo imekuja baada
ya kuwepo nongono kuwa Maalim Seif amechoka na nafasi ya Makamu wa Kwanza na anataka
kupewa Juma Duni na ndipo akaamua kumpeperusha na kumpelekeka CHADEMA.
Kiongozi huyo alilaani hatua iliyochukuliwa na CUF
ya kuwatoa viongozi wao katika Baraza la Wawakilishi huku akieleza athari za
kutoka kwao katika kikao hicho ambacho kilikuwa kinapitisha Bajeti ya Serikali.
Alieleza kuwa katika kipindi cha miaka mitano Dk.
Shein amefanya kazi kubwa sana katika kuleta mabadiliko makubwa na kujenga
misingi imara ya maendeleo na anafaa kuwa Rais, na kuwahakikishia Wazanzibari
kuona Zanzibar mpya katika uongozi wake wa miaka mitano ujao kwani ana mipango
kabambe ya kuondosha umasikini na kuongeza ajira kwa vijana.
Nae Balozi Ali Karume aliwaomba wananchi wa Pemba
kumpa kura zao Dk. Ali Mohamed Shein kutokana na kuwa na uwezo, uzoefu na
kueleza kuwa mgombea wa CUF hamfikii Dk. Shein.
Bi Mauwa Daftari nae alieleza mafanikio
yaliopatikana katika kuimarisha miradi ya maendeleo ikiwemo maji, barabara,
umeme na mengineyo na kueleza jinsi anavyomfahamu Dk. Shein kuwa ni muadilifu,
mchapakazi na hana tabia ya kusema uongo.
Alisema kuwa Sera za CCM ni kuwasikiliza wananchi shida
zao na kuzifanyia kazi huku akisema anamfahamu sana Dk. Magufuli kwani amefanya
kazi nae pamoja na sifa zake zinafanana
na za Dk. Shein na kueleza kuwa akipigiwa Dk. Shein akina mama nao
tayari wameshapata nafasi kupitia Mama Samia Suluhu Hassan.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kaskazini Pemba Hamad
Mberwa, akiwakaribisha viongozi na WanaCCM pamoja na wananchi katika Mkoa huo alisema
kuwa Pemba ya mwaka 1995,2000 na 2010 sio ya leo na wananchi wake wamebadikila,
kimawazo na kivitendo. Kampeni rasmi za CCM zilifunguliwa siku ya Jumaapili
tarehe 13.
Rajab
Mkasaba, Ikulu Zanzibar
Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail:
rajabmkasaba@yahoo.co.uk
No comments:
Post a Comment