Haya ndiyo Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu (Ajenda 2030) ambayo leo Ijumaa Wakuu wa Nchi na Serikali wanayapitisha katika Mkutano wao wa Kihistoria Unaofanyika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani. Anjenda 2030 ambayo utekelezaji wake unaaza mwakani inachukua nafasi ya Malengo ya Maendeleo ya Millenia( MDGs) ambayo yamefikia ukiongoni mwaka huu. Upitishaji wa Ajenda 2030 utatanguliwa na hotuba ya Baba Mtakatifu Francis 

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula akizungumza wakati wa mkutano ulioandaliwa kwa pamoja na Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani na Mashirika ya Kimataifa kama vile Mpango wa Chakula Duniani, Mkutano uliokuwa ukijadili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na uhusiano wake na usalama wa chakula, lishe na afya. Mkutano huu ulifanyika siku ya alhamis katika Uwakilishi wa Kudumu wa Ujeruman katika Umoja wa Mataifa
Sehemu ya washiri wa mkutano kuhusu uhusiano wa mabadiliko ya tabia nchi na athari zake kwa usalama wa chakula, lishe na afya wakimsikiliza Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula ambaye alikuwa kati ya wanajopo watano waliozugumza katika mkutano huo
No comments:
Post a Comment