Habari za Punde

Umoja wa Mataifa Leo Kuandika Historia Nyengine.

Haya ndiyo  Malengo Mapya ya Maendeleo Endelevu (Ajenda 2030) ambayo  leo Ijumaa Wakuu wa Nchi na Serikali wanayapitisha katika Mkutano wao wa Kihistoria  Unaofanyika  Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York Marekani. Anjenda 2030 ambayo utekelezaji wake unaaza mwakani inachukua nafasi ya  Malengo ya Maendeleo ya Millenia( MDGs) ambayo yamefikia ukiongoni mwaka huu.  Upitishaji wa Ajenda 2030 utatanguliwa na hotuba ya Baba Mtakatifu Francis 
Katibu Mkuu  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Balozi  Liberata Mulamula akizungumza wakati wa mkutano ulioandaliwa  kwa pamoja  na  Wizara ya Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani na Mashirika  ya Kimataifa kama vile Mpango wa Chakula Duniani, Mkutano uliokuwa ukijadili changamoto za mabadiliko ya tabia nchi na uhusiano wake na usalama wa chakula,  lishe na afya. Mkutano huu ulifanyika  siku ya alhamis katika Uwakilishi wa Kudumu wa Ujeruman katika Umoja wa Mataifa
Sehemu ya washiri wa mkutano  kuhusu uhusiano wa mabadiliko ya tabia nchi na athari zake kwa usalama wa chakula,  lishe na afya wakimsikiliza Katibu Mkuu, Balozi Liberata Mulamula ambaye alikuwa kati ya wanajopo watano waliozugumza katika mkutano huo



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.