Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai akizungumza na waandishi wa habari kukanusha habari zinazosambazwa katika mitandao ya Kijamii kuhusuana na mazungumzo yanayoendelea kwa Viongozi wa Zanzibar, Na kusema kauli hizo ni za uongo hazina ukweli wowote na kusema mazungumzo yanaendelea na wanasubiri siku ya Tume ya Uchaguzi kutangaza tarehe ya kurudia Uchaguzi na wao wako tayari kushiriki uchaguzi huo wa marudio.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM kisiwandui.
No comments:
Post a Comment