Habari za Punde

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Alaani Vitengo Vya Baadhi ya Watu Kusambaza Habari za Uongo Katika Mitandao ya Kijamii.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar Ndg Vuai Ali Vuai akizungumza na waandishi wa habari kukanusha habari zinazosambazwa katika mitandao ya Kijamii kuhusuana na mazungumzo yanayoendelea kwa Viongozi wa Zanzibar, Na kusema kauli hizo ni za uongo hazina ukweli wowote na kusema mazungumzo yanaendelea na wanasubiri siku ya Tume ya Uchaguzi kutangaza tarehe ya kurudia Uchaguzi na wao wako tayari kushiriki uchaguzi huo wa marudio. 
Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali vilioko Zanzibar  katika ukumbi wa Afisi Kuu ya CCM kisiwandui.





No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.