Habari za Punde

Jamuhuru ya Watu wa China Kupitia Jimbo la Jiangsu Yatowa Msaada wa Dawa wenye Thamani ya Zaidi ya Shilingi Milioni 500 kwa SMZ.

Balozi mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xie Yunliang akitoa maelezo wakati wa sherehe ya kukabidhi msaada wa dawa zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 500 zilizotolewa na  Jimbo la Jiangsu kwa ajili ya Wananchi wa Zanzibar. Sherehe hiyo ilifanyika Bohari Kuu ya Madawa  Maruhubi Mjini Zanzibar.
Baadhi ya Madaktari wa China na waalikwa wakifuatilia sherehe ya makabidhiano ya msaada wa dawa  mbali mbali za binaadamu katika sherehe iliyofanyika Bohari Kuu ya Madawa Maruhubi.
Kamishna wa Afya na Uzazi wa Mpango ambae pia ni Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Jimbo la Jiangsu Hong Hao akizungumza wakati wa makabidhiano ya dawa zenye thamani ya shilingi milioni 500 (kulia) Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabiti Kombo.
 Balozi mdogo wa China aliyepo Zanzibar Xie Yunliang na Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo wakitia saini makabidhiano ya dawa hizo zilizotolewa na Jimbo la Jiangsu.
 Naibu Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo na Balozi mdogo wa China wakibadilishana hati za makabidhiano ya msaada wa dawa zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 500 katika sherehe zilizofanyika Bohari Kuu ya Madawa Maruhubi.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.