Habari za Punde

Rais wa Zanzibar Dk Shein, Waapisha Mkuu wa Wilaya ya Micheweni na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Nd,Abeid Juma Ali kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba,kabla ya uteuzi huo alikuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar,hafla ya kiapo  ilifanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akimuapisha Nd,Ali Khamis Juma  kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha kabla aklikuwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Uwezeshaji Uataswi wa Jamii Vijana Wanawake na Watoto Zanzibar,hafla ya kiapo hicho ilifanyika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
Baadhi ya Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa Mkuu mpya wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini Pemba Nd,Abeid Juma Alina Naibu Katibu Mkuu Wizara ya FedhaNd,Ali Khamis Juma leo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu mpya wa Wilaya ya Micheweni Mkoa wa Kaskazini PembaNd,Abeid Juma Ali (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Nd,Ali Khamis Juma (kulia)baada ya kuwaapisha kushika nyadhifa hizo katika ukumbi wa Ikulu Mjini Unguja.{Picha na Ikulu}  
STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
 Zanzibar                                                                                                            7.12.2015
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein leo amemuapisha  Ndugu Abeid Juma Ali, kuwa Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Pemba.

Wakati huo huo, Dk. Shein amemuapisha ndugu Ali Khamis Juma, kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria katika hafla hiyo ni Dk. Mwinyihaji Makame Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Ikulu na Utawala Bora, Waziri wa Fedha Mhe. Omar Yussuf Mzee, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Idara Maalum Mhe. Haji Omar Kheir, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassn Said .

Wengine ni Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Mhe. Abdalla Mwinyi Khamis, Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji, Naibu Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh  Hassan Othman Ngwali, Meya wa Manispaa ya Mji wa Zanzibar Khatib Abrahman Khatib,Washauri wa Rais wa Zanzibar na viongozi wengine wa Serikali.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822 
 E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.