Habari za Punde

Kituo cha Sheria Zanzibar Chatowa Elimu ya Katiba kwa Wanafunzi wa Pemba.

Afisa Mdhamini Elimu Pemba, Salum Kitwana Sururu akifungua mafunzo ya utayarishaji wa Katiba na sheria kwa wanafunzi wa skuli za sekondari Pemba, amabao ni wanachama wa vilabu kadhaa kisiwani humo, kulia ni Mratibu wa mafunzo hayo Mohamed Hassan Ali na kushoto ni Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar tawi la Pemba, Fatma Khamis Hemed
Fatma Khamis Hemed wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, akiwaonyesha katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, wanafunzi wa skuli za sekondari Pemba, ambao ni wanachama wa vilabu mbali mbali, ikiwa ni pamoja na mazingira na sayansi, kwenye mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria
Mratibu wa mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria Mohamed Hassan Ali, akiwa makini kusikiliza michango ya wananfunzi ambao ni wanachama wa vilabu kadhaa, akifuatiwa na Aisa Mdhamini elimu, Salum Kitwana Sururu.
Wanafunzi wa vilabu kadhaa ikiwa ni pamoja na sayansi wa skuli za sekondari Pemba, wakisikiliza mada zilizowasilishwa kwenye mafunzo yalioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC kisiwani Pemba, juu ua utayarishaji wa katiba na sheria

Mtoa mada Mohamed Hassan Ali, akiwasilisha mada juu ya haki za binadamu, kwa wanafunzi wa skuli za sekondari ambao ni wanachama wa vilabu kadhaa, mafunzo hayo yalioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, na yalifanyika afisini kwao mjini Chakechake
Khalfan Amour Mohamed wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, akiwasilisha mada ya udhalilishaji, kwa wanafunzi wa skuli za sekondari Pemba, ambao ni wanachama wa vilabu mbali mbali ikiwa ni pamoja na mazingira na sayansi, kwenye mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria
Mwanafunzi anaesoma darasa la kumi (FII), skuli ya Connecting Chakechake, akielezea namna ambayo mafunzo ya utayarishaji wa katiba na sheria, jinsi atakavyo yafikisha kwa wanafunzi wenzake na jamii kwa ujumla, (Picha na Haji Nassor, Pemba).  

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.