Habari za Punde

Wananchi wa Michamvi Kupata Maji Safi na Salama Ikiwa ni Matunda ya Mapinduzi.

Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar

Jumla ya Wananchi 1,572 wa Vijiji vya Michamvi Pingwe na 

Michamvi Kae wanatarajiwa kupata Maji safi na salama 

baada ya kukamilika kwa Mradi wa kuchuja Maji Chunvi 

kuwa Maji matamu.

Kukamilika kwa mradi huo kutawapunguzia Kero wananchi 

wa Vijiji vya Michamvi ambao kwa miaka mingi 

wamekumbwa na tatizo hilo bila ya msaada wowote.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Uwezeshaji, ustawi wa 

Jamii,Vijana Wanawake na Watoto Zanzibar Zainab Omar 

Mohammed wakati akiweka Jiwe la Msingi la Mradi huo 

huko Michamvi wilaya ya Kusini Unguja.

Amesema uwekaji wa Jiwe la Msingi wa Mradi huo na 

kupata maji matamu ambayo yatawasaidia wananchi hao ni 

moja kati ya jitihada zinazofanywa na Serikali ya Mapinduzi 

Zanzibar kwa lengo la kuwaondoshea shida ya upatikanaji 

wa maji wananchi wake.

“Malengo makubwa ya jitihada hizo ni kuwaondoshea kero 

Wananchi ya kukosekana kwa huduma hiyo ya maji safi ili 

waweze kushughulikia zaidi kazi za uzalishaji mali na 

maendeleo kwa lengo kuimarisha kipato chao” amesema 

Waziri Zainab.

Ameongeza kuwa eneo la Michamvi ni moja kati ya maeneo 

yanayokabiliwa na upatikanaji wa maji safi na salama na 

kwamba baada ya muda mfupi wananchi wataondokana na 

kero hiyo.

Akitoa taarifa juu ya Mradi huo Naibu Katibu mkuu Wizara 

ya Ardhi, Makaazi,Maji na Nishati Mustafa Jumbe amesema 

Mradi umetekelezwa na kugharamiwa kati ya Serikali ya 

Mapinduzi Zanzibar na Kampuni ya UST kutoka Ujerumani 

ambapo jumla ya Shilingi Millioni 475 za Kitanzania 

zinatarajiwa kutumika.

Amefafanua kuwa Kampuni ya UST imechangia Milioni 395 

ambapo kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi kwa 

kushirikiana na Wananchi wamechagia Millioni 80.

Jumbe amezitaja kazi zitakazofanyika kuwa ni pamoja na 

uchimbaji wa kisima,utiaji wa pampu,ujenzi wa kibanda cha 

kuwekea mitambo na ununuzi wa mitambo ya kusafishia 

maji chumvi kuwa matamu.

Akitoa nasaha Mkuu wa Wilaya ya Kusini Jabir Khamis 

Makame amewaomba wananchi wa Michamvi kuuenzi Mradi 

huo ili uweze kuwaletea matunda yaliyokusudiwa.

Uwekaji wa Jiwe la Msingi Mradi wa Kuchuja maji Chumvi 

kuwa Maji matamu ni moja ya matunda ya Mapinduzi ya 

Zanzibar ambayo lengo lake ni kuwakombo Wananchi na 

Umasikini ikiwemo kuwaletea maji safi na salama katika 

maeneo yao.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.