Shirikisho la kabumbu barani Afrika(CAF)
limewateuwa waamuzi wenye beji za FIFA kutoka
nchini Djibouti kuchezesha pambano la awali kati ya
Sports Club Villa Jogoo ya Uganda dhidi JKU ya
Zanzibar.
Kupitia Shirikisho lao la mpira nchini Uganda (FUFA)
Sports Club Villa tayari wamethibitisha kuwa
pambano hilo litachezwa kwenye dimba la kimataifa
la Mandela Jumamosi ya March 12 saa kumi alasiri.
Waamuzi hao ni Souleiman Ahmed Djamal, Abdillahi
Mahamoud Iltireh, Hamze Abdi Salime, Djamal Aden
Abdi na Kamisaa wa mchezo huo atakua Aweis
Ahmed Jumal kutoka nchini Somalia.
Sports Club Villa imetinga hatua hiyo baada ya
kuitoa Al Khartoum ya Sudan kwa ushindi wa jumla
ya 2-0 kufuatia michezo miwili waliocheza.
Kwa upande wao JKU walifanikiwa kuingia nafasi
hiyo bila ya jasho kutokana na wapinzani wao
Gaborone United kutoka Botswana kujiengua kwenye
kombe hilo la Shirikisho barani Afrika.
No comments:
Post a Comment