Habari za Punde

Masauni ziarani mkoani Kigoma

 Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (katikati), akisalimiana na wafanyakazi wa Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa yanayohudumia wakimbizi katika Kambi ya muda ya NMC, iliyoko mkoani Kigoma, kushoto ni Mratibu wa Wakimbizi  Mkoani  Kigoma, Tonny  Samwel  Laiser.Naibu Waziri yupo mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani Ofisi ndogo ya Kibondo,Dost Yousafzai (kushoto), akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), wakati ya ziara ya Naibu Waziri kutembelea ilipokuwepo kambi ya wakimbizi ya Karago, wilayani Kibondo. Naibu Waziri yuko mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.
Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wakimbizi wa Burundi (hawapo pichani) wanaoishi katika kambi ya Mtendeli, iliyoko wilayani Kakonko mkoani Kigoma.Naibu Waziri yuko Mkoani Kigoma kwa ziara ya kikazi.(Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi)

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.