Habari za Punde

Waandishi wa Habari Zanzibar na Wananchi Wapata Elimu ya Kijikinga na Kipindipindu.

Mkurugenzi  Mtendaji Kamisheni ya Maafa Zanzibar ndugu  Ali Juma  Hamad akifungua mafunzo ya waandishi wa habari juu ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupindu katika Ukumbi wa gereji ya Wizara ya Afya Mombasa Mjini Zanzibar, (kulia) daktari dhamana Kanda ya Unguja Dkt Fadhili Mohd na (kushoto) Mwakilishi wa WHO Zanzibar Dkt. Ghirmay.
Washiriki wa mafunzo hayo wakimsikiliza  kwa makini Daktari dhamana Kanda ya Unguja Dkt. Fadhili Mohd alipokuwa akielezea njia za kukabiliana na kipindupindu katika mafunzo  ya siku moja yaliyofanyika Ukumbi wa  Gereji ya Wizara ya Afya Mombasa Mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo Zanzibar Rafii Haji Mkame akiwasilisha mada ya wajibu wa waandishi wa habari katika kukabiliana na maradhi ya miripuko katika mafunzo yaliyofanyika Ukumbi wa Gereji ya Wizara ya Afya Mombasa Mjini Zanzibar.
Katibu wa Jumuiya ya Maafisa wa Afya Zanzibar Ahmed Suleiman Said akitoa elimu ya kupambana na maradhi ya kipindupindu kwa wananchi wa shehia ya Shaurimoyo Mjini Zanzibar.
Baadhi ya wananchi wa shehia ya Shaurimoyo Mjini Zanzibar wakifuatilia juu ya elimu ya ugonjwa wa Kipindupindu iliyotolewa na Jumuiya ya Maafisa wa Afya Zanzibar.
Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.