Habari za Punde

Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar Yakamata Shehena ya Mafuta ya Kupikia Yaliyoingizwa Nchini Kinyume na Sheria Yakiwa Karibu Kumaliza Muda Wake kwa Matumizi ya Binadamu.

Wafanyakazi wa Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar wakifungua Godauni lenye mafuta ya kupikia yanayokaribia kumaliza muda wake wa matumizi ya kula binadamu, eneo la Amani magogoni Mjini Zanzibar.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Premium Enterprises Ndg.Humud Nassor Humud akiyakagua ili kuyatambua madumu ya kampuni yake ambayo yamekamatwa na Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar yakitumiwa na wafanyabiashara wasio waaminifu kutia mafuta ya kupikia yanayokaribia kumaliza muda wake ili yaonekane kuwa ni mapya.
Shehena ya maboksi ya mafuta ya kula yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria.

Mkuu wa Idara ya Usalama na Ubora wa Chakula wa (ZFDB) Bi. Aisha Suleiman akizungumza na wandishi wa habari kuhusu kukamatwa mafuta yaliyoingizwa nchini kinyume na sheria yenye thamani ya miliono 40.
(Picha na Makame Mshenga-Maelezo Zanzuibar.)

2 comments:

  1. Kwa hili niwapongeze sana kwani afya zetu ni muhimu adhabu Kali ifuatie kwa mfanyabiashara asie mwaminifu

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.