Habari za Punde

Daraja la Kigamboni, Watanzania Wafarajika, Mamia Waenda Kuliangalia

 Daraja la ksiasa la Kigamboni linalounganisha eneo la Kigambonina upande wa Kurasini likikatisha bahari ya Hindi. Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kulizindua rasmi daraja hilo Jumanne Aprili 19, 2016. (Picha na K-VIS MEDIA/Khalfan Said)


NA K-VIS MEDIA/Khalfan Said, Kurasini
ZAMANI kwa mgeni aingiae jiji la Dar es Salaam, ataambiwa “Kashangae Ferry” lakini mgeni atakayeingia leo jijini, ataambiwa Kashangae Kurasini-daraja la Kigamboni.
Hiyo ndiyo hali halisi ilivyokwa sasa ambapo mamia yawakazi wa jiji wamekuwa wakienda kwenye Daraja la kisasa la Kigamboni mosi kushangaa maajabu ya daraja lenyewe ambalo ni refu kuliko madaraja yote hapa nchini pengine Afrika Mashariki, lakini pili kupiga picha za kisasa “Selfie”.
Daraja hilo lenye urefu wa mita 680 likiunganisha eneo la Kigamboni na Kurasini wilayani temeke jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa za wakandarasi wa mradi huo, Daraja hilo litakuwa na barabara sita, tatu kila upande, na pia njia za waenda kwa miguu (Pedestrians).
Hali pametengwa milango kwa ajili ya matumizi ya magari aina tofauti.
Geti namba 1 ni kwa wale wenye vibali maalum, geti namba 2 geti namba 3 na geti namba 4 ni wenye magari madogo binafsi, geti namba 5 ni mini bus (daladala) na Geti namba 6 nimaalum kwa malori.
Daraja hilo ambalo ujenzi wake umeanza Februari 1, 2012 ni mradi wa ubia kati ya Serikali yenye asilimia 40 naMfuko wa Hifadhi ya Jamii, NSSF yenye asilimia 60.
Daraja hilolinaongeza vivutio vikuu viwili ambavyo wilayaya Temeke jijini Dar es Salaam inavyo, daraja lenyewe la Kigamboni lakini pia uwanja wa kisasa wa taifa.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli anatarajiwa kulizindua rasmi daraja hilo umanne Aprili 19, 2016 na tayari maandalizi ya hafla hiyo yanaendelea ambapo K-VIAS MEDIA, imezuru eneo hilo leo Aprili 18, 2016 na kujionea wajkandarasi namaafisa wa serikali wakiweka mambo sawa tayari kwa shughuli hiyo muhimu katika historia ya nchi hii.
Lakini pia ukitaka kuona mfano wa “Flyover” basi pitia hapo Kurasini uone jinsi barabar zilivyobebana kuelekea eneo la daraja na zile zinazoungana na barabara ya Mandela.



 Akina mama hawa na watoto wao walikuwa ni miongoni mwa wakazi wa jiji la Dar es Salaamwanaofika kulishangaa daraja hilo la kisasa
Barabara inayoelekea kwenye daraja hilo

1 comment:

  1. Namshukuru Mungu BABA kwa maendeleo ya nchi yetu! Wote wanaoiwazia mema na kuchukua hatua kuijenga wapewe fadhili na Mungu BABA katika Jina la Yesu...Mungu BABA apitishe kusudi lake kwa Rais Magufuri na Serikali yake

    ReplyDelete

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.