Mwalimu Yussuf Shoka Hamad
alipokabidhi vifaa kwa Mwalimu mkuu shule ya msingi Simai, Wingwi, Mw. Muhammed
Hamad pamoja na Walimu wengine wakiwa katika picha ya pamoja
Mwalimu Yussuf Shoka Hamad akikabidhi vifaa kwa
Mwalimu Khamis Rashid wa Shule ya Msingi Wingwi
Na: Waandishi kutoka Pemba
Shule za msingi Mtemani, Wingwi
msingi na Simai zote za Wingwi, wilaya ya micheweni mkoa wa kaskazini Pemba,
zimepatiwa msaada wa vifaa vya kisasa vya kutendea kazi kwa ajili ya kuleta
ufanisi kazini.
Msaada
huo uliotolewa na mhadhiri kutoka chuo
kikuu cha SOAS, London, nchini Uingereza
Mwalimu Yussuf Shoka Hamad, ulijumuisha mashine ya kompyuta za dawatini,
mashine ya kutolea fotokopi, kupigia skani na kuchapishia barua na hati mbali
za kiofisi.
Katika
hafla fupi iliyoandaliwa na shule hizo jana (Jumatatu) mchana, Bwana Yussuf
alisema kuwa lengo na nia yake ni kuzisaidia shule zote za Wingwi kwa kuzipatia vitendea kazi vya kisasa
ili kukuza ufanisi na kuendana na maendelea ya sasa ya dunia ya sayansi na
teknolojia.
‘Lengo
langu si kujijenga kisiasa. Mimi si mwanasiasa, naruadia kusema hivi na
naisitiza tena kwamba sitoi misaada hii kwa madhumuni ya kisiasa. Mimi ni
mzaliwa wa Wingwi na ari ya uzawa na
mchango nilioupata kwa jamii yangu ya Wingwi ni miongoni mwa misukumo
inayonipelekea kutoa misaada hii bila kuchoka na bila kujali thamani, ukubwa au
udogo wa vitu hivyo ninavyotowa’.
Bwana
Yussuf pia aliongezea kwa kusema nia yake hasa ni kuzibadilisha shule zote za
Wingwi na kuzifikisha katika kiwango cha ubora wa shule za kisasa kivitendea
kazi ifikapo mwaka 2020. Moja kati ya mikakati yake ya kufikia lengo hilo ni
kuhakikisha kila shule inapata mashine za kutolea kopi (photokopi) zenye uwezo
wa kuchapisha mitihani ya ndani ya wanafunzi, kujenga maktaba za ndani ya shule
hizo na kuzipa uwezo wa vifaa vya asili na vile vya kisasa ili kukuza kiwango
cha elimu nchini.
Katika
hafla hiyo, Bwana Yussuf aliahidi kuzipatia shule hizo mashine za kutolea
photokopi (kubwa) ifikapo mwakani ambapo kila shule itaweza kujitegemea kwa
vitendea kazi vyenye uwezo na ubora wa
kisasa.
Wakitoa
shukrani zao kwa Mwalimu huyo, Walimu wakuu wa shule hizo walimpongeza Mwalimu Yussuf kwa uzalendo
na moyo wake wa kujitolea na hasa katika
kusaidia sekta ya elimu ya shule hizo za Wingwi.
‘Kwa
kweli msaada huu ni mkubwa kwetu kiasi ambacho hatujui jinsi gani tufikishe
shukrani zitakazofikia thamani ya msaada huu. Tunashukuru sana na tunakutakia
heri na fanaka katika kazi zako ili uweze kusaidia zaidi katika sekta hii ya
Elimu ya shule zako za Wingwi.’ Aliema Mwalimu Mohammed Hamad wa Shule ya
Msingi Simai.
Naye
Mwalimu mkuu msaidizi wa Shule ya msingi Wingwi, Bwana Khamis Rashid
alimshukuru na kumpongeza Bwana Yussuf Shoka kwa hatua yake hiyo ya kukumbuka
kusaidia shule za Wingwi ambako yeye (Yussuf) alisomea hapo.
Msaada
huu wa zawadi uliotolewa ni moja ya sehemu za ahadi alizitowa Bwana Yussuf
wakati wa hafla ya kuwazawadia wanafunzi waliofaulu mitihani yao ya darasa la
saba mwaka jana ambapo kiwango cha ufaulu kwa wanafunzi wa shule hizo
kimeongezeka maradufu katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.
No comments:
Post a Comment