Wafanyakazi wa kampuni
ya simu ya Zantel leo wameshiriki katika zoezi la kupanda miti kwenye hifadhi
ya Masingini iliyopo magharibi mwa kisiwa cha Unguja kama moja ya jitihada zake katika kutekeleza mpango
wa kutunza na kuhifadhi mazingira visiwani Zanzibar.
Eneo la hifadhi ya msingini lipo
mita 120 kutoka usawa wa bahari na ni eneo lenye vyanzo vingi vya maji ambavyo vinakadiriwa kutoa lita 27,400,000 kwa ajili
ya matumizi ya kila siku ya wakazi wa Zanzibar.
Akizungumza wakati wa upandaji miti,
Afsa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya simu ya Zantel,bwana Benoit Janin alisema
kupanda miti kutasaidia kuzuia mmomonyoko wa ardhi, kuongeza rutuba ya udongo na pia kulinda vyanzo vya
maji .
‘Kama Kampuni ya
simu inayotoa huduma ya mawasiliano kwa wakazi wa visiwani ni lazima
tuhakikishe tunatunza na kuhifadhi mazingira kama moja ya rasilimali muhimu kwa ajili ya ustawi wa jamii yetu’alisema Bw
Janin.
Zoezi hili la
kupanda miti limefanyika leo, ikiwa ni wiki moja tu toka uzinduzi wa mtandao wa
4G visiwani hapa, hatua inayoonyesha kuwa kampuni ya Zantel imejipanga katika
mpango wa kuhakikisha inalinda na kuhifadhi mazingira kwa kushirikiana na
serekali yetu .
Akizungumza baada ya tukio hilo,
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mazingira Zanzibar, bwana Sheha
Mjaja Juma aliwapongeza wafanyakazi wa kampuni ya simu ya Zantel kwa kuweza kushiriki kwenye zoezi hilo la kutunza na kuhifadhi mazingira.
‘Madhumuni
ya zoezi hili la upandaji miti hapa Masingini yamelenga kusaidia jitihada za kutunza
na kulinda vyanzo vya maji, msitu pia kuzuia mmonyoko wa ardhi ili kulinda
viumbe hai vilivyopo kwenye eneo hilo’ alisema bwana
Sheha.
No comments:
Post a Comment