Na, Himid Choko
BLW
WAFANYAKAZI wa Afisi ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar,
wameiomba Serikali pamoja na Wajumbe wa
Baraza hilo, kuridhia na hatimae kuiipitisha Sheria ya Utawala wa Baraza ili kuleta ufanisi wa utendaji ndani ya Afisi
hiyo.
Wafanyakazi
hao wametoa ombi hilo leo, wakati wa mkutano wa pamoja wa kujadili Utendaji wa kazi , mkutano ambao
pia umehudhuriwa na Spika wa Baraza hilo Mhe Zubeir
Ali Maulid na Naibu Spika Mhe.
Mgeni Hassan Juma.
Mmoja
ya Wanyakazi hao Makame Salim wa Sehemu
ya Taarifa Rasmi za Baraza amesema
Sheria ya Utawala wa Baraza ambayo kwa sasa imeshapelekwa Serikalini ,
endapo itakubalika itasaidia kwa kiasi kikubwa
kulifanya Baraza kuepukana na changamoto mbali mbali za kiutendaji ndani
ya muhimili huu wa Dola.
Amesema
kuwa miongoni mwa faida zitakazopatikana baada ya kupitishwa sheria hii ni Uhuru
wa Baraza wa kujiendesha na
kujiamulia mambo yake wenyewe kama
yalivyo Mabunge mengi ya nchi za Jumuiya ya Madola.
“Hata
Baraza na Ofisi ya baraza la Wawakilishi kwa jumla, linakabiliwa na changamoto
kadhaa, lakini ikipatikana Sheria hii ya Utawala ya Baraza asilimia kubwa ya
changamoto hizi zinaweza kutatuliwa, na jambo hili sio geni kwani mabunge ya Jumuiya ya madola yamekuwa
yakiendeshwa kwa mfumo kama huu” alimalizia ndugu Makame.
Wamesema
Sheria hiyo pia itasaidia kuiwezesha
Ofisi ya Baraza kuwa na uwezo wa
kuwasimamia watumishi wake katika njanja
za maslahi, wajibu na adhabu pale wanapokwenda kinyume na utaratibu wa majukumu
yao ya kazi.
Aidha
Wafanyakazi hao wamesisitiza kuangalia
upya maslahi yao ukizingatia mazingira
nyeti ya kuwahudumia wanasiasa na kutunza siri za serikali.
‘Mhe
Spika, kwa kweli tunafanya kazi katika mazingira magumu na nyeti, tunawahudumia
viongozi na wanasiasa na tunatunza siri nyingi, kama maslahi yetu yataendelea
kuwa kama haya nafasi kama hii inaweza kutumiwa na wafanyakazi wasiokuwa
waaminifu kutumika vibaya na watu wengine wasiopendelea mafanikio ya nchi yetu”
Alisisitiza Sulum Mkubwa wa Divisheni ya hansard ya Baraza la Wawakilishi.
Mkuu
wa divisheni ya Utafiti na maktaba ya baraza la wawakilishi, Othaman Ali Haji
amemuomba Spika kupigania Upatikanaji wa Fursa hizo kama vile elimu na kozi za
muda mfupi hasa nnje ya nchi kama vile zinavyopatokana katika taasisi nyengine
serikalini.
Nae
Spika Maulid ameahidi kushirikiana na
wafanyakazi hao na kusimamia maslahi yao na kuwaomba kuzidisha umoja na
mashirikiano katika utendaji wao wa majukumu yao ya kazi.
Amesema katika kuimarisha mahusiano mema ya kikazi atajenga tabia ya kukutana na
wafanyakazi hao mara kwa mara ili
kushauriana , kuelekezana na kukosoana
kwa lengo kuhimiza wajibu na uwajibika kati ya Viongozi wa Baraza, Afisi ya
Baraza na watumishi wa Afisi hiyo.
No comments:
Post a Comment