Habari za Punde

Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, Azindua Kisima cha Maji na Uzinduzi wa Msikiti Katika Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja.

Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, akizindua kisima cha Maji Safi na Salama kwa Wananchi wa Kijiji cha Umbuji na msikiti wa Kijiji hicho anayeshuhudia Mwalim 
Shekh Khamis. 
Balozi  wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem,akionja maji baada ya kuzindua kisima cha maji kwa ajili ya Msikiti wa Umbuji Wilaya ya Kati Unguja na Wananchi wa Kijiji hicho kulia Shekh Khamis.
Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, akiwa na Shekh Khamis Abdalla baada ya uzinduzi wa kisima hicho cha Maji Safi na Salama katika Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja Mkoa wa Kusini Unguja.
Jengo la Msikiti Mpya baada ya kujengwa upya kwa msaada wa Africa Muslim Agency Zanzibar, katika Kijiji cha Umbuji Zanzibar Wilaya ya Kati Unguja. 
Wananchi wa Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati wakihudhuria katika uzinduzi wa msikiti wao mpya baada kujengwa upya. 
Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, akitembelea kijiji cha umbuji Wilaya ya Kati Unguja wakati wa haflaya uzinduzi wa msikiti na kisima cha maji safi na salama.

Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al Najem akizungumza na mwananchi wa kijiji cha umbuji wakati wa ziara yake ya uzinduzi wa kisima cha maji na uzinduzi wa masikiti katika kijiji hicho cha umbuji Zanzibar.
Balozi Jasem Al Najem akikata utepe kuashiria Uzinduzi wa Jengo Jipya la Msikiti wa Kijiji cha Umbuji Zanzibar Wilaya ya Kati Unguja.



Wananchi wa Kiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja wakisoma dua baada ya kumaliza kusali sala ya alasiri baada ya uzinduzi wa msikiti huo.
Mwananchi wa Kijiji cha Umbuji akisoma ratiba uzinduzi wa msikiti wa kijiji cha Umbuji wakati wa uzinduzi wa msikiti huo uliofanywa na Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al Najem. 
Maalim wa Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja akisoma Quran wakati wa hafla ya uzinduzi wa msikiti huo katika Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja Mkoa wa Kusini Zanzibar.
Wananchi wa Kijiji cha Umbuji wakimsikiliza msoma Quran wakati wa uzinduzi huo.
Mwananchi wa Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja Mkoa wa Kusini Zanzibar akisoma risala ya Wananchi wakati wa hafla ya uzinduzi wa msikiti huo.
Shekh akitowa mawaidha kwa Wananchi wa Kijiji cha Umbuji wakati wa Uzinduzi wa Msikiti huo na kutowa nasaha kwa Wananchi wa Kijiji cha Umbuji Zanzibar. wakati wa Uzinduzi wa Msikiti wa Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja. 
Mkurugenzi Mkuu wa Africa Muslims Agency Zanzibar, akizungumza na kumkaribisha Balozi wa Kuwait kuzungumza na Wananchi wa Kijiji cha Umbuji Wilaya ya Kati Unguja.
Balozi wa Kuwait Nchini Tanzania Balozi Jasem Al-Najem, akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Umbuji Unguja wakati wa hafla ua uzinduzi wa Kisima cha Maji na Uzinduzi wa Msikiti, katika Kijiji hicho baada ya kujengwa upya kwa msaada na Africa Muslims Agency Zanzibar.hafla hiyo imefanyika katika kijiji hicho huko umbuji Zanzibar. 






No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.