Habari za Punde

Ligi ya Vijana Wadogo Yafikia Tamati Wilaya ya Mjini Unguja. Mbunge wa Chumbuni Mhe Ussi Pondeza (AMJAD) Mgeni Rasimin Katifa Fainali Zilizofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar.

Viongozi wa jukwaa kuu wakifuatilia mchezo wa fainal wa kufunga michuano ya Vijana Wadogo Wilaya ya Mjini Unguja yaliofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar na kukabidhiwa zawadi za Makombe na Fedha Taslim Washindi wa michezo hiyo. 
Mgeni Rasmin wa Fainali za Ligi za Vijana Wadogo Wilaya ya Mjini Central League Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza (AMJAD) akiwahutubia wanamichezo wakati wa hitimisho la michuano hiyo kufikia tamati kwa kupatikana washindi na kuwakabidhi zawadi zao, na kukubali ombi lao la kuwa mlezi wa Michuano hiyo ya Vijana Wadogo wa Wilaya ya Mjini, na kuahidi kuimarisha michezo katika Wilaya hiyo na kusema Michezi ni Ajira kwa Vijana.
Viongozi wa ZFA Wilaya ya Mjini Unguja wakiwa katika hafla hiyo ya Fainali ya Michezo ya Vijana Wilaya ya Mjini Unguja yaliofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar.
Viongozi wa Vilabu na ZFA wakifuatilia hutuba ya Mgeni Rasmin Mhe Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza.(AMJAD)

Mbunge wa Jimbo la Chumbuni akimvisha Medeli Mchezaji Bora wa Juniuor Hassan Ali 
Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Mhe Ussi Salum Pondeza (AMJAD) akimkabidhi kikombe na madeli mchezaji bora Said Salum. 
Vijana Wapenzi wa mchezo wa mpira Visiwani Zanzibar wakifuatilia utowaji wa zawadi kwa Washindi wa Michuano ya Vijana Wadogo wa Wilaya ya Mjini Unguja katika uwanja wa amaan Zanzibar.
Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza(AMJAD) akimkabidhi fedha na kikombe mchezaji bora wa Vijana Wadogo Yussuf Mohammed kwa kuwa mchezaji Bora kwa mwaka huu.
Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza (AMJAD) akimkabidhi Kombe Nahodha wa Timu ya AZM AFC Zanzibar Mudasir Abdalla.

Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar akimkabidhi Kombe Nahodha wa Timu ya Real Said Salum. 
Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Ussi Salum Pondeza (AMJAD) akimkabidhi Kombe Nahodha wa Timu ya AFC Boys Salum Khamis. 




Mwenyekiti wa ZFA Wilaya ya Mjini Unguja Hassan Chura akimvisha Nishani ya Heshima ya Ulezo wa Michuano ya Vijana Wadogo wa Wilaya ya Mnjini Unguja Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe Miraji Khamis Mussa. 
Mwenyekiti wa ZFA Wilaya ya Mjini Unguja Hassan Chura akimvisha nishani ya Heshima ya Ulezi wa Michuano ya Ligi ya Vijana Wadogo Wilaya ya Mjini Unguja Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Zanzibar Mhe. Ussi Salum Pondeza (AMJAD) wakati wa hafla ya hitimisho la micuano ya Ligi ya Vijana Wadogo Wilaya ya Mjini Unguja.   

Mwenyekiti wa ZFA Wilaya Mjini Unguja Ndh Hassan Chura akizungumza na kutowa shukrani kwa Kamati ya Ligi ya Vijana Wagodo Wilaya ya Mjini kwa kukamilisha Michuano hiyo na kufikia tamati kwa kukabidhiwa zawadi washindi. na Kumpongeza Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Chumbuni kukubali kuwa Walezi wa Michuano ya Ligi ya Vijana Wadogo wa Wilaya ya Mjini Unguja.
Mgeni Rasmin Rainali za Ligi za Central League Wilaya ya Mjini Mbunge wa Jimbo la Chumbuni Mhe Ussi Salum Pondeza (AMJAD) na Mwakilishi wa Jimbo hilo Mhe. Miraj Khamis Mussa wakiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Central League Wilaya ya Mjini wakati wa fainali za michuano hiyo kwa Vijana zilizofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar. 28-5-2016. 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.