Habari za Punde

Risala ya mahafali ya tatu ya Al -Ihsaan Girls Secondary School

AL-IHSAAN GIRLS SECONDARY SCHOOL
RISALA YA MAHAFALI YA TATU YA WANAFUNZI WA KIDATO CHA SITA 2016
MHESHIMIWA MGENI RASMIN. WAZIRI WA `BIASHARA, VIWAANDA NA MASOKO, BALOZI AMINA SALUM ALI.

MHESHIMIWA BALOZI WA KUWAIT NCHINI TANZANIA, MR JASSEM IBRAHIM AL – NAJIM

NDUGU MKURUGENZI WA SHIRIKA LA AFRICA MUSLIM AGENCY MR. AIMAN MOH’D

MWENYEKITI WA  KAMATI YA SKULI, NDUGU VUAI MUSSA.

MWALIMU MKUU WA SKULI YA AL-IHSAAN,  NDUGU ABUBAKAR AHMAD MWADINI.

NDUGU MAAFISA WA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI

NDUGU VIONGOZI WA ZAPS

MHESHIMIWA MWAKILISHI WA JIMBO LA M/KWE

WAHESHIMIWA MASHEHA NA MADIWANI WA WADI NA SHEHIA ZA MWANAKWEREKWE NA MAGOGONI.

WAGENI WAALIKWA,

NDUGU WANAFUNZI

MABIBI NA MABWANA ITIFAKI INAZINGATIWA

Asalamu alykum Warahmatullah Wabarakatuh

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Awali ya yote, napenda kumshukuru allah (S.W) kwa kutujaalia uhai na uzima kwa kutuwezesha kukutana hapa katika siku hii ya leo.

Pili, kwa niaba ya walimu na wanafunzi wenzangu naomba nitumie nafasihii kukushukuru wewe mgen rasmin, kwa kukubali kushirikiana nasi katika mahafali yetu ya tatu ya kidato cha sita.

Licha ya majukumu yako mazito ya kitaifa, hii inazihirisha wazi kwamba upo pamoja nasi kukamilisha sherehe hizi hasa kwa nafasi yako ya kitaifa wewe ni mlezi na kwetu ni kiongozi wa wizara ya biashara, viwanda na masoko, aidha tunapenda kutumia nafasi hii kuwashukuru wazazi wetu kwa mahudhurio yao.

Muheshimiwa mgeni rasmin.

Kihistoria, skuli hii ya wasichana imeanzishwa na shirika Afrika Muslim Agency, February 2002 ikiwa na madarasa manane, vyumba viwili vya walimu, ofisi ya mwalimu mkuu, maabara moja, chumba cha maktaba, chumba cha chai na vyoo ishirini na sita (26). Na mwalimu mkuu wa mwanzo, alikua marehemu Bi Maryam Omar Moh’d,  ambaye aliongoza skuli kwa takriban miaka saba (7).

Shule ilianza na jumla ya wanafunzi 89 wa kidato cha kwanza na walimu sita (6), katika kipindi cha uongozi wake, marehemu Bi Maryam alisisitiza sana suala la nidhamu ya wanafunzi kwa wanafunzi, walimu kwa walimu na baina ya walimu na wanafunzi. Aidha, mafanikio ya jitihada zake yalionekana baada ya kipindi kifupi ambapo wanafunzi wa mwanzo waliofanya mitihani ya taifa kidato cha nne mwaka 2005 na mwaka 2007, kufikia asilimia mia matokeo yao, matunda ya jitihada zake, busara na hekima zake baada ya kipindi kifupi cha uongozi wake nabado matokeo mazuri yanaendelea kupatikana hadi sasa sio tu kwa masomo lakini pia kitabia za walimu na wanafunzi.


Mheshimiwa mgeni rasmin.

Kuanzia mwaka 2005 hadi mwaka 2015, shule imetoa wahitimu 554 wa kidato cha nne, ambapo 548 walifaulu na kupata vyeti, sawa na silimia 98.91, aidha kati ya wanafunzi 548 waliopata vyeti, wanafunzi 296 wamefaulu kuendelea kidato cha tano na sita, hii ni sawa na asilimia 54.01. mafanikio haya yamepelekea wazazi na wanafunzi kuleta watoto wao kwa wingi, hivi sasa shule ina jumla ya wanafunzi 450 na walimu 25 kati yao wanawake 9 na wanaume 16

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Jengo jipya liliopo upande wa kulia la madarasa sita na maabara mbili, limewezesha kuanzishwa kidato cha tano na sita kuanzia mwaka 2012 hii ni pamoja na ongezeko  la vifaaa vya maabara ambavyo shirika linagharamia, vilevile kwa sasa shule haina upungufu wa vikalio nikiwa na maana viti, meza na madawati.

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Kwa upande wa kidato cha tano na sita, hadi kufikia mwaka 2016, shule imeshatoa wanafunzi 88 kwa mikupuo mitatu. Kwa mkupuo wa mwanzo mwaka 2012-2014 kati ya wanafunzi 20 waliofanya mitihani ya kidato cha sita ya mwaka 2014 wanafunzi 19, sawa na asilimia 95 walifaulu na kupata vyeti vya kidato cha sita na wamejiunga na vyuo vikuu mbali mbali nchini. Mwaka 2015 idadi ya watahiniwa walikua 21, ambapo jumla ya wanafunzi 20 walifaulu na kujiunga na vyuo mbali mbali na kwa mwaka huu tupo jumla ya wahitimu 47 ambao wapo mbele yako na kwa sasa tunasubiri matokeo yetu ili tujiunge na vyuo mbali mbali biidhini llah.


Mheshimiwa mgeni rasmin.

Kama hayo hayatoshi Shirika linadhamini wanafunzi wote wanaojiunga na kidato cha tano na sita ndani ya skuli yetu kwa wale wanaofaulu kwa ngazi ya daraja la kwanza na la pili katika mitihani ya “O” level kudhaminiwa  masomo ya juu advance, hii inatupa faraja sisi wanafunzi na inatia moyo na kutupa ari sisi wanafunzi kuongeza bidii ili kunufaika na fursa hii adhimu na ya ghali.  Pamoja na ufadhili huo pia shirika linaendeleza ufadhili wa kuwafadhili sare za skuli kwa wanafunzi yatima na wenye hali ngumu. Aidha tunapenda kulishukuru na kulipa pongezi shirika la Africa Muslims Agency kwa kuongeza nguvu ya msaada wa chakula kwenye maandalizi ya mitihani yetu.

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Fursa nyengine ambayo wanafunzi wanaipata wanaofaulu na kuwa na sifa za kujiunga vyuo wanapeewa fursa nyengine ya kudhaminiwa masomo yao ya juu.

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Penye mafanikio hapakosi changamoto, katika maisha yetu ya kidato cha kwanza hadi cha sita tumekabiliwa na changamoto tatu kuu, kwanza kukosa dahalia ambapo wanafunzi wanaweza kuishi kwa muda wote ili kuwawezesha wanafunzi kujisomea kwa muda wote, uzowefu unaonesha kwamba shule nyingi zenye dahalia O level na advance matokeo yao yanakua mazuri ukilinganisha na zile ambazo hazina dahalia, pili, uwezo mdogo wa wazazi wa kuchangia huduma za chakula, tatizo hili limepelekea wanafunzi kukaa muda mdogo kambini, tatu, tatizo la mara kwa mara la kuharibika kwa miundombinu ya maji.


Mheshimiwa mgeni rasmin.

Tunatoa shukurani za dhati kwa Mwalimu mkuu maalimu Abuu Bakar Ahmad na viongozi wenzake kwa jitihada zao na moyo wao wa kuongoza skuli kwa hekima na busara ambazo zimesaidia kutatua changamoto mbali mbali siku hadi siku. Aidha tunawashukuru walimu wetu wa masomo kwa juhudi zao za kutupa taaluuma pamoja na malezi mazuri.

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Vile vile tunatoa shukurani zetu kwa mwalimu mkuu mstaafu mwalimu Ibrahim Marine kwa uongozi wake wa busara na hekima tangu mwaka 2009-2015, pia tunamshukuru mlezi wetu na mshauri wetu wa skuli mama yetu Bi Mgeni Moh’d Said, bila ya kusahau uongozi wa skuli wakiwemo Bi Yusra Juma, Maalimu Omar Halfan, Maalim Rashid Dadi na Maalim Abdallah Nassor kwa kuwa nasi bega kwa bega kipindi chote cha kambi tulichokuwepo hapa skuli

Mheshimiwa mgeni rasmin.

Tunaomba utukubalie tena shukurani zetu na tunakushukuru kwa kuwacha kazi zako na kujumuika nasi.

Mwisho tunamuomba Allah atupe kila la kheri wewe na sisi pamoja na walimu wetu na wazazi wetu na wanafunzi wenzangu. AAMIN

Ahsanteni kwa kunisikiliza



No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.