Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe. Dr. Abdallah Possi ( Mb) akizungumza wakati wa majadiliano ya jumla kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Haki za Watu wenye Ulemavu. Mhe. Possi anaongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Tisa wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Watu Wenye Ulemavu. Mkutano huu wa siku tatu umeanza siku ya Jumanne hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Wajumbe wengine katika picha ni kutoka kushoto Mhe. Stella Ikupa Alex ( Mb), Mhe. Riziki Said Lulida ( Mb) na Mhe Elly Marko Macha ( MB).
Ujumbe wa Tanzania wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Tisa wa Mkataba wa Watu Wenye Ulemavu, ufunguzi wa mkutano huu ulifanyika katika Ukumbi Mkuu wa Mikutano ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Mkutano huu wa siku tatu ajenda yake ni "Utekelezaji wa Agenda ya Maendeleo Endelevu ( Agenda 2030) Kwa Watu Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”. Unahudhuriwa na Washiriki kutoka nchi 164 ambazo zimeridhia Mkataba huu, Asasi zisizo za kiserikali pia zinahudhuria katika mkutano huu ambao ni maalum kwa watu wenye ulemavu wa aina zote.
Na Mwandishi Maalum, New York
Mkutano wa
Tisa wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za
Watu Wenye Ulemavu(CRDP),umeanza jana (Jumanne)
hapa
Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa,
New York, Marekani.
Mada au ujumbe wa Mkutano huu wa siku tatu ni “
Utekelezaji
wa Agenda ya Maendeleo Endelevu (Agenda2030) Kwa
Watu
Wote Wenye Ulemavu: Pasipo Kumwacha Yeyote”
Ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Mkutano
huu, unaongozwa na Naibu
Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Mhe.
Dr.Abdallah Possi(Mb). Wajumbe wengine ni Mhe.
Riziki Lulinda( MB), Mhe. Elly Macha (Mb) Mhe. Stella Ikupa (Mb), Bi
Josephine Lyengi, Kaimu Kamishna kuhusu watu wenye ulemavu na Bi.Ngusekela Nyerere,Afisa Mambo ya Nje, Wizara ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Akizugumza wakati wa majadiliano ya jumla mara baada ya hafla
ya ufunguzi
, Naibu Waziri. Dr. Abdallah Possi amesema,
changamoto kubwa inayowakabili watu wenye ulemavu nchini
Tanzania, ni fursa za kiuchumi.
“Licha ya mafanikio kadhaa yakiwamo ya utungaji wa
sera, sheria
na mabadiliko mbali mbali kuhusu watu wenye ulemavu,
bado
kunachangamoto nyingi ambazo zinatakiwa kufanyiwa kazi kwa
lengo la
kuwapunguzia matatizo watu wenye ulemavu yakiwamo
matatizo ya kutokuwa na fursa sawa na kuondokana na
umaskini”. Akaeleza Naibu Waziri
Na
Kuongeza kwamba, Tanzania kama ilivyo kwa nchi yingine
inakabiliwa pia
na vipaumbele vinavyokinzana na ambavyo ni
muhimu lakini vikiwa athiri zaidi watu wenye ulemavu.
Akavitaja baadhi ya vipaumbele hivyo kuwa ni pamoja na
upatikanaji wa maji safi na salama,
chakula, huduma za afya,
elimu na ukosefu wa ajiria.
Vile
vile Naibu Waziri
ameeleza kuwa mtazamo husika kuhusu
watu wenye ulemavu ni changamoto nyingine ambayo inatatiza
ujumuishwaji wa watu wenye ulemavu katika fursa mbali mbali za
maendeleo ya kiuchumi na kijamii ambazo wangeweza kunufaika
nazo bila ya kujali hali zao.
Akizungumzia kuhusu mahitaji ya watu wenye ulemavu nchini
Tanzania, Mhe. Dr.Possi,
ameeleza washiriki wa mkutano huu
kutoka nchi 164 ambazo zimeridhia mkataba wa watu wenye
ulemavu kwamba, watu wenye ulemavu nchini Tanzania
wanakabiliwa na tatizo kubwa la
kutokuwa na vifaa saidizi
ambavyo vingewasaidia na kuwawezesha katika shughuli zao za
kila siku.
ya wadhamini wakuu wa Azimio kuhusu watu wenye ualibino,
azimio ambalo pamoja na mambo
mengine limelenga katika
kutafutia ufumbuzi baadhi ya changamoto zinazowakabili watu
wenye ualibino katika maeneo mbali mbali yakiwamo ya elimu,
afya na ajira.
“Bila ya kuwa na vifaa saidizi watu wenye ulemavu wa aina
yoyote ile wanashindwa kupata fursa ambazo kwa kuwawezesha kuishi pasi utegemezi na hivyo kuchangia katika yao binafsi na maendeleo ya nchi yao”
akasisitiza Naibu Waziri. Na akatumia fursa hiyo ya kuhimiza upatikanaji wa vifaa saidizi kwa watu wenye ulemavu ili waweze kujitegemea.
Awali akifungua mkutano wa tisa wa Mkataba wa Watu Wenye
Ulemavu, Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,
Bw.Mogens Lykketoft,
amesema nchi ambazo zimeridhia mkataba huo zinaowajibu wa kuchukua hatua zote muhimu zikiwamo za maendeleo jumuishi kwa watu wenye ulemavu.
“Kila nchi mwanachama wa mkataba huu na asiye wamanachama
anakazi ya kufanya,
lakini katika dunia ya leo mafanikio hayamo
katika mikono ya serikali peke yake”
akasisitiza Rais wa Baraza
Kuu la Umoja wa Mataifa.
Na
kwa sababu hiyo ametoa wito kwa serikali zote pamoja na
wadau mbali mbali kufanyakazi kwa pamoja kwa lengo
la
kuwawezesha watu wenye ulemavu zaidi ya bilioni moja.
Pamoja na hotuba kutoka kwa nchi wanachama,
mkutano huu
ambao ni wa siku tatu utakuwa na mijadala ya mapendekezo yenye
mada tofauti. Mkutano huo pia unashirikisha Asasi zisizo za
kiserikali zinazojihusisha na masuala ya watu wenye ulemavu.
No comments:
Post a Comment