Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akizungumza na wananchi wa Jimbo hilo wakati wa mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Jimbo ambapo alitoa taarifa juu ya watu wazima kuanzia umri wa miaka 70 kupata huduma ya matibabu bure
Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni, Zanzibar wakimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (hayupo pichani) wakati akizungumza katika mkutano uliofanyika katika Ofisi ya Jimbo ambapo alitoa taarifa juu ya watu wazima kuanzia umri wa miaka 70 kupata huduma ya matibabu bure
Meneja wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Tawi la Zanzibar, Ismail Kangeta, akitoa ufafanuzi juu ya huduma ya matibabu itakayoanza kutolewa bure kwa wananchi wa Jimbo la Kikwajuni, wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo.Wapili ni Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni
Mwananchi wa Jimbo la Kikwajuni akisoma kipeperushi kilichotolewa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ambacho kina majina ya Hospitali ambazo wafaidika wa huduma ya matibabu bure wanaweza kwenda kupata huduma hiyo wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo hilo Kikwajuni Zanzibar
Mbunge wa Jimbo la Kikwajuni ambae pia ni Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni(kulia), akimsikiliza mmoja wa wananchi wa Jimbo hilo mara baada ya kutoa muda wa kusikiliza kero mbalimbali za wananchi wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo hilo, Zanzibar
Mwakilishi wa Jimbo la Kikwajuni, Nassor Salim
Jazeera (kulia), akimsikiliza mwananchi wa Jimbo hilo mara baada ya kutoa muda
wa kusikiliza kero mbalimbali za wananchi
wakati wa mkutano uliofanyika Ofisi ya Jimbo hilo, Zanzibar.
No comments:
Post a Comment