Mkurugenzi wa Taasisi
ya Sayansi na Teknolojia ya Karume, Bwana Haji Abdulhamid akimuonyesha baadhi
ya vitabu vilivyopo katika maktaba ya taasisi, Mkurugenzi Mtendaji wa Zantel,
Bwana Benoit Janin. Anayetazama kulia ni Mkuu wa Zantel upande wa Zanzibar,
Mohamed Mussa.
Mkurugenzi wa Taasisi
ya Sayansi na Teknolojia ya Karume, Bwana Haji Abdulhamid (katikati) akionyesha
ramani mpya ya taasisi ya Karume. Kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja, bwana
Idrissa Muslih Hijja na kutokea kushoto ni Mkuu wa Zantel upande wa Zanzibar,
Mohamed Mussa akifuatiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Zantel, Bwana Benoit Janin
(kulia).
•
Yazindua ofa mpya ya gharama nafuu kwa wanafunzi wa vyuo vikuu
Zanzibar, Juni 3, 2016:
Kampuni ya simu inayoongoza visiwani Zanzibar, Zantel leo imetoa msaada wa vitabu
vya uhandisi kwa Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Karume vyenye thamani ya
shilingi milioni 10 kama sehemu ya jitihada zinazofanywa na kampuni hiyo
kumaliza tatizo la uhaba wa vitabu katika taasisi ya Karume na kusaidia utoaji
wa elimu bora.
Taasisi
ya Karume ilianzishwa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uhandisi kwa fani
mbalimbali ikiwemo mafunzo ya ufundi wa magari, umeme, kompyuta, mawasiliano na
teknolojia ya uchukuzi.
Afisa
Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Zantel, Bwana Benoit Janin alisema msaada huo umelenga
kusaidia taasisi ya Karume kuendelea kukuza taaluma yake ya mafunzo kwa kupunguza
tatizo la uhaba wa vitabu vya kujifunzia.
'Vitabu
ni muhimu kwa ajili ya kuongeza maarifa na hivyo basi msaada huu utasaidia Taasisi
hii kuendelea kutoa elimu bora na kuwahakikishia wanajumuiya wa chuo hiki upatikanaji
wa dhana za kujifunzia kwenye mafunzo yao' alisema Bw.Janin.
Akizungumza
katika hafla ya makabidhiano, Mkurugenzi wa Taasisi ya Karume, Bwana Haji Abdulhamid
aliishukuru kampuni ya Zantel kwa msaada wake akisema umekuja wakati muafaka kwani
taasisi yake imekuwa inakabiliana na changamoto za uhaba wa vitabu kwa ajili ya
kukidhi mahitaji ya wanafunzi zaidi ya 1,500 ilionao sasa.
'Swala
la uhaba wa vitabu katika chuo chetu limechangia kupungua kwa ufaulu na uelewa
katika masomo ya sayansi ’ alisema Bwana Haji Abdulhamid.
Pamoja
na kukabidhi msaada huo, kampuni ya Zantel pia imeanzisha mpango maalumu wa
kushirikisha wafanyakazi wake kwa kutoa semina kwa wanafunzi ili kubadilishana
mawazo na kuwaongezea ujuzi na uzoefu wanafunzi walio vyuoni.
Pamoja
na makabidhiano ya msaada kampuni ya Zantel pia imezindua huduma mpya kwa ajili
ya wanafunzi wa vyuoni ili kuweza kukidhi mahitaji yao ikiwemo kupata gharama
nafuu za kupiga simu, kutuma ujumbe pamoja na mtandao na hivyo kuboresha na
kuimarisha mazingira ya kujifunzia.
'Ofa hii ni kwa ajili ya wanafuzi wa vyuoni imezingatia
uwezo wao kiuchumi kwa kuzingatia kipato chao pamoja na mahitaji na matumizi,
lakini lengo haswa ni kuwapunguzia gharama ili kuwapa thamani ya fedha zao' alisema
Bw.Janin.
ili
kufurahia huduma hiyo mwanafunzi atatakiwa awe na laini ya Zantel na kujisajili
kwa kutumia kitambulisho chake cha chuo kisha apige *149*1 # kujiunga.
No comments:
Post a Comment