Habari za Punde

Ujumbe wa Jiangsu kutoka China wakutana na Dk Shein leo ikulu

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Katibu wa Chama cha Kikoministi cha China kutoka Kamati ya Jimbo la Jiangsu Bw.Luo Zhijon,(kulia) akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo jioni,[Picha na Ikulu.] 02/06/2016.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Katibu wa Chama cha Kikoministi cha China kutoka Kamati ya Jimbo la Jiangsu Bw.Luo Zhijon,(kulia) akiwa na ujumbe wake walipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo jioni,[Picha na Ikulu.] 02/06/2016.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na Ujumbe wa Chama cha Kikoministi cha China kutoka Kamati ya Jimbo la Jiangsu ukiongozwa na Katibu wake  Bw.Luo Zhijon,(kushoto) mara  ujumbe huo ulipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo jioni,[Picha na Ikulu.] 02/06/2016.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Ali Mohamed Shein akizungumza na Ujumbe wa Chama cha Kikoministi cha China kutoka Kamati ya Jimbo la Jiangsu ukiongozwa na Katibu wake  Bw.Luo Zhijon,(wa tatu kulia) mara  ujumbe huo ulipofika Ikulu Mjini Zanzibar leo jioni,[Picha na Ikulu.] 02/06/2016.


STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
  Zanzibar                                                        2.06.2016
---
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ametoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa kuendelea kuiunga mkono Zanzibar katika kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo ikiwemo sekta ya afya.

Dk. Shein aliyasema hayo leo katika mazungumzo kati yake na Katibu wa Chama cha Kikomunisti cha China katika Kamati ya Jimbo la Jiangsu Bwana Luo Zhijun akiwa amefuatana na ujumbe wake uliofika Ikulu mjini Zanzibar.

Katika mazungumzo hayo, Dk. Shein alisema kuwa azma ya Jimbo la Jiangsu kuendeleza mashirikiano yake kwa kuimarisha sekta mbali mbali za maendeleo nchini ni hatua moja wapo ya kukuza uhusiano wa kidugu uliopo kati ya pande mbili hizo.


Dk. Shein alipongeza azma ya Kiongozi huyo katika kuimarisha uhusiano katika sekta ya afya, elimu, viwanda, uekezaji, utalii pamoja uvuvi kati ya Zanzibar na Jimbo hilo la Jiangsu.

Aidha, Dk. Shein alieleza kuwa Zanzibar itaweza kufaidika kwa kiasi kikubwa na makubaliano ya awali juu ya mafunzo kwa madaktari na wauguzi wazalendo kati yake na Jimbo hilo, kwani ni hatua kubwa katika kuhakikisha sekta ya afya inaimarika hapa nchini.

Dk. Shein alitumia fursa hiyo kutoa pongezi na shukurani kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kupitia Jimbo la Jiangsu kwa  utamaduni wa kuendelea kuwaleta Madaktari bingwa kutoka Jimbo hilo tokea mwaka 1964, ambapo mbali ya wataalamu hao pia, nchi hiyo imeweza kuleta wataalamu wake mbali mbali  hapa Zanzibar.

Aidha, Dk. Shein alitoa shukurani kwa chama cha Kikomunisti cha China kwa kuendeleza ushirikiano wake na chama tawala cha CCM na kuahidi kuendeleza mashirikiano hayo kwa kupanua wigo katika nyanja mbali mbali za maendeleo.

Dk. Shein alisema kuwa ziara zinazofanywa na viongozi wakuu wa vyama hivyo katika nchi mbili hizo zimeweza kuzidisha mashirikiano makubwa yaliopo ambayo ni ya kihistoria.

Dk. Shein pia, alitumia fursa hiyo kueleza uhusiano na ushirikiano uliopo kati ya Jimbo hilo na Zanzibar na kuahidi kuendelezwa na kudumishwa, huku akisisitiza kuwa China imeweza kutoa mchango mkubwa katika mafanikio ya sekta mbali mbali hapa Zanzibar.

Pamoja na hayo, Dk. Shein alitoa pongezi zake kwa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China chini ya kiongozi wake Rais Xie Jingping kwa kuendelea kuisaidia na kuiunga mkono Zanzibar katika kuendeleza miradi mbali mbali ya maendeleo ukiwemo ujenzi wa Bandari, Hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani Pemba, Ujenzi wa Uwanja wa Mao tse Tung na ujenzi wa jengo jipya la abiria katika uwanja wa ndege wa Abeid Amani Karume Zanzibar.

Nae Kiongozi huyo wa Jimbo la Jiangsu katika maelezo yake, alieleza azma ya ziara yake hapa Zanzibar kuwa ni pamoja na kusaini makubaliano ya awali ya mashirikino katika sekta ya afya baina ya Hospitali za Jimbo hilo ikiwemo Hopitali ya Chuo Kikuu cha Nanjing na Hospitali ya Mnazi MMoja.

Aidha, kiongozi huyo alisema kuwa ujio wake una lengo la kusaidia vifaa vya tiba na madawa hasa katika matibabu ya akina mama wajawazito na wanawake.

Kiongozi huyo alitumia fursa hiyo, kumpongeza Dk. Shein pamoja na chama chake cha CCM kwa ushindi mkubwa uliopatikana katika uchaguzi mkuu uliopita na kuahidi kuendelea kutoa mashirikiano kwa chama hicho kwa lengo la kuendeleza udugu na mashirikiano yalioanzishwa na waasisi wa mataifa hayo.

Sambamba na hayo, Kiongozi huyo alieleza kuwa ushirikiano na uhusiano kati ya Zanzibar na China ni wa kihistoria ambapo Jimbo la Jiangsu lilianza kutoa ushirikiano wake kwa kuleta madaktari hapa Zanzibar tokea mwaka 1964.

Pamoja na hayo, Kiongozi huyo alimuahidi Dk. Shein kuwa Jimbo lake litaimarisha ushirikiano katika sekta ya viwanda vikiwemo viwanda vya nguo,
mashirikiano katika sekta za kiuchumi hasa katika bidhaa za baharini, uvuvi pamoja na sekta ya utalii.

Pia, Kiongozi huyo alimuahidi Dk. Shein kuwa mashirikiano zaidi yataimarishwa katika sekta ya elimu ikiwa ni pamoja na utoaji wa mafunzo kwa madaktari, wauguzi, mafunzo ya vyuo vya amali pamoja na ufundi.

Kwa upande wa sekta ya uwekezaji kiongozi huyo alimuahidi Dk. Shein kuwa Jimbo lake litatoa mashirikiano zaidi katika kuimarisha sekta ya uvuvi kwa kuanzisha viwanda vya uvuvi hasa kutokana na Jimbo hilo kupata mafanikio makubwa katika sekta hiyo.

Pamoja na hayo, Kiongozi huyo alimueleza Dk. Shein kuwa China inatoa nafasi nyingi za ufadhili wa masomo hivyo alisisitiza haja kwa Wazanzibari kujiunga na vyuo vikuu vilivyomo Jimbo hilo.

Kiongozi huyo pia, alisisitiza haja ya kuimarisha mashirikiano na uhusiano uliipo kati ya Jamhuri ya Watu wa China na Tanzania ikiwemo Zanzibar.

Rajab Mkasaba, Ikulu Zanzibar

Postal Address: 2422 Tel.:0777427449. Fax: 024 2231822
E-mail: rajabmkasaba@yahoo.co.uk

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.