Habari za Punde

ZLSC Pemba waandaa mkutano wa kisheria kwa shehia ya Mgagadu

 WANANCHI wa shehia ya Mgagadu Jimbo la Chambani, wilaya ya Mkoani Pemba, waliohudhuria mkutano wa kupokea msaada wa kisheria bila ya malipo, kutoka kwa watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 AFISA Mipango wa Kiuto cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Khalfan Amour Mohamed, akifafanua jinsi wanavyotoa msaada wa kisheria bila ya malipo, wakati watendaji wa Kituo hicho na baadhi ya wanasheria, walipofika shehia ya Mgagadu wilaya ya Mkoani kutoa msaada huo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
 NAIBU sheha wa shehia ya Mgagadu Kassim Juma Makame, akifungua mkutano maalumu wa kutoa msaada wa kisheria, kwa wananchi wake, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, kulia ni Naibu Mwenyekiti wa mahakama ya ardhi Chakechake, Pemba Salim Hassan Bakar na kushoto ni Mratib wa ZLSC Pemba Fatma Khamis Hemed,(Picha na Haji Nassor, Pemba).
 MRATIBU wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba, Fatma Khamis Hemed, akifafanua kuhusu kosa la ubakaji kisheria, kwenye mkutano wa kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi wa shehia ya Mgagadu wilaya ya Mkoani Pemba, katikati ni Naibu sheha wa shehia ya Mgagadu Kassim Juma Makame na kulia ni Naibu Mwenyekiti wa mahama ya ardhi Chakechake Pemba Salim Hassan Bakar, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

 KHADIJA Omar Msellem wa shehia ya Mgagadu akiuliza kuhusu suala la uchangiaji wa huduma ya maji safi na salam kisheria ikoje, kwenye mkutano wa msaada wa kisheria, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, tawi la Pemba na kufanyika shehiani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).
MWANAFUNZI wa skuli ya Mizingani wilaya ya Mkoani Pemba, Rashid Omar Mohamed akitaka ufafanuzi wa kuchelewa kwa kesi za ubakaji, kwenye mkutano wa msaada wa kisheria, ulioandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, tawi la Pemba na kufanyika shehiani humo, (Picha na Haji Nassor, Pemba).

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.