Habari za Punde

Dk Shein safarini Uingereza

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
    Zanzibar                                                       26 Julai, 2016

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein ameondoka leo kwenda nchini Uingereza kwa ziara maalum ya wiki mbili.

Katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Dk. Shein, ambaye amefuatana na mke wake Mama Mwanamwema, aliagwa na viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo mawaziri, Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Makatibu Wakuu na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi anatarajiwa kurejea nchini mara baada ya kumalizika ziara hiyo.

Postal Address: 2422 Tel.+255 776 613 015, Fax: 024 2231822 

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.