Na
Maryam Kidiko/Kijakazi Abdalla-Maelezo Zanzibar
Serikali
ya Mapinduzi ya Zanzibar imesema lengo kuu la kufanywa tamasha la Utamaduni wa
Mzanzibar ni kuwaunganisha wazanzibar katika kulinda na kudumisha utamaduni huo.
Hayo
yameelezwa mshauri wa Raisi katika mambo ya utamaduni Chimbeni Kheri katika
ufungaji wa tamasha la 21la utamaduni wa mzanzibar huko Fukuchani Wilaya ya
kaskazini A”.
Amesema
kuwa utamaduni huo pia unawakutanisha wazanzibar kutoka sehemu mabali mbali ili
waweze kubadilishana mawazo juu ya njia bora ya kuendeleza utamaduni kupitia
njia ya sanaa.
Aidha
amesema utamaduni ni roho ya taifa hivyo unahitaji kuenziwa , kuendelezwa,
kurithiwa na watoto wetu katika michezo mbali mbali ya kiutamaduni .
“
Utamaduni ni muhimu sana kwani hujenga afya ,kukuwa kwa kiakili na hupata ajira
kwani dunia ya sasa inazingatia sekta ya sanaa na utamaduni katika ustawi wa
maendeleo ya kimataifa.Alisema Chimbeni.
Hata
hivyo ameeleza kuwa majanga mengi katika jamii hujitokeza kwa kuacha mila na
desturi za kizanzibar hivyo kuna umuhimu mkubwa wa kuurejesha utamaduni wetu .
Sambamba
na hayo amesema kuwa Serikali imeweka mazingira mzuri yakuwawezesha Wasanii wa fani zote ili kuweza kunufaika na
kazi zao ili kuweza kuchangia pato la taifa .
“Katika
suala la utamaduni serikali imechukuwa hatua madhubuti ikiwa ni pamoja na kuifanyia
marekebisho sheria inayohusu mambo ya utamaduni ili iendane na mahitaji ya
Jamii” Alisema mshauri huyo.
Nae
Waziri waHabari Utalii Utamaduni na Michezo Rashid Ali Juma amesema Wizara yake
itashirikaana na Wizara ya elimu kuhakikisha somo la utamaduni linarudi katika
skuli ili watoto waweze kuzijuwa mila na utamaduni wao .
Waziri
huyo amefafanuwa zaidi kuwa suala la utamaduni litaendelea kuwepo na kuwa la kihistoria na kila
mmoja anatakiwa kuwa balozi wa mwenziwe ili kuweza kuulinda utamaduni huo
usipotee katika visiwa vyetu.
Sambamba
na hayo Tamasha hilo limejumuisha michezo mbalimbali ya kiutamaduni ambapo
kauli mbiu ya mwaka huu ni Dumisha utamaduni na amani , piga vita udhalilishaji
.
No comments:
Post a Comment