Habari za Punde

Spika Zubeir ahudhuria Mkutano wa CPA Mauritius.






Spika wa Baraza la Wawakilishi  Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid yuko nchini Mauritius kuhudhuria Mkutano wa 47 wa  Umoja wa  Mabunge ya Nchi za Jumuiya ya Madola  Kanda ya Afirika (CPA African Region).

Mkutano huo ulioanza Ogasti 22 na kutarajiwa kumalizika Ogasti 27 unafanyika katika hoteli ya Intercontinental Balaclava Mauritius ambapo unahudhuriwa  na washiriki wapatao 400 kutoka nchi  wanachama 20, chini ya mwenyeji wao  Spika wa nchi hiyo   Bibi Santi Bhai Hanoomajee ambae  kwa sasa  ndie Rais wa Jumuiya hiyo kikanda.

Tanzania, Afrika ya Kusini , Msumbiji, Uganda  na Kenya  ni miongoni mwa  nchi zinazoshikiriki katika mkutano huo ambapo  pamoja na Spika wa Baraza la Wawakilishi Mheshimiwa Zubeir Ali Maulid,  mshiriki mwengine kutoka Zanzibar ni Mwakilishi wa Tunguu Mheshimiwa Simai Mohammed Mpakabasi .

Miongoni mwa mada zinazojadiliwa  katika mkutano huo ni pamoja na Uwezeshaji wa wanawake kiuchumi ikiwa ni miongoni mwa mkakati wa kupunguza umasikini pamoja na nafasi ya  Mabunge katika kudumisha  haki, amani na ushiriki  mzuri wa jamii katika shughuli za kisiasa.

Mada nyengine zinazozozungumzwa ni ustawi wa jamii  kiafya, kimazingira na kielimu pamoja namaendeleo ya vijana  na kuichumi miongoni mwa nchi wanachama.

Awali Mheshimiwa Spika Zubeir na Mheshimiwa Simai Mpakabasi walihudhuria  Mkutano wa Kamati Tendaji  ambao ulipitia agenda mbali mbali za Mkutano Mkuu.

Zanzibar ni mwanachama  wa CPA African Region, ambapo Baraza la Wawakilishi  limekua likishiriki  mara kadhaa  katika mikutano, semina na mafunzo yanayoandaliwa na jumuiya hiyo.


Imetolewa na

Divisheni ya Uhusiano,
Baraza la Wawakilishi,
Zanzibar.

August 25, 2016

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.