Na salmin Juma Pemba
Serikali imeombwa kukifufua kitengo cha idara ya ushirika
wizara maalum au kama kipo basi kiweze kusimama na kufanya wajibu wake kwa
kuona umuhimu wa uwepo wa vikundi vya ushirika katika jamii na hasa kwa kuwa
vyama vya ushirika vya mkowa vipo.
Hayo yamesemwa hapo jana na mwenyekiti mpya wa chama kikuu
cha ushirika mkoa Kusini Pemba (MKOCHA) Bw: Nassor Suleiman Nassor mara baada ya uchaguzi mkuu wa chama hicho
kupitia mkuuhuko katika ukumbi wa skuli ya maandalizi Chanjaani njia ya
airport.
Amesema ni vyema serikali ikarejesha kitengo hicho kwa kuwa
ndio mlezi mkuu wa vyama vya ushirika ili kufanya wajibu wake na malengo
yaliyokusudiwa kupitia vyama hivyo kuweza kufikiwa.
Amesema malengo makuu ya vyama vya ushirika ni kuona wananchi
kupitia vyama hivyo wanajikwamua kimaisha na kuondokana na umasikini na kupiga
hatua za kimaendeleo ila bado amesema serikali inaonekana haijatilia nguvu
uwepo wa vyama hivyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi nje ya kikao hicho
Mgeni rasmi katika ghafla hiyo bw: Kassim Ali Omar afisa mipango ofisi ya mkuu
wa wilaya chake, amesema amelipokea shauri hilo na amesema atalifikisha katika
ngazi husika na kukaa na viongozi wengine kulijadili suala hilo ili kuona siku
moja linasimama na kufanikiwa.
Kupitia mkutano huo uliweza kufanyika uchaguzi mkuu kwa
viongozi mbali mbali wa chama hicho kikuu cha ushirika mkoa MKOCHA Na
kufanikiwa kupatikana kwa mwenyekiti mpya na wajumbe 7 wa bodi ya mkoa na
wajumbe 3 watakaowakilisha mkutano mkuu taifa.
No comments:
Post a Comment