Habari za Punde

Makampuni ya Ericsson na Huawei wakabidhi vifaa vyenye thamani ya Tsh.Bilioni 2 kwa ajili ya kuboresha mitambo na huduma za mawasiliano ya Zantel.

 Alex Kamamia  wa Ericsson (wa pili kulia) akielezea jinsi mtambo mpya wa mawasiliano ya Zantel utakavyoboresha huduma kwa watumiaji wa mtandao wa Zantel. Wakimsikiliza ni Mkuu wa Ufundi wa Zantel Larry Arthur (kushoto) na Jx Chen wa Huawei (wa pili kushoto) na Frode Dyrdal (kulia) wa Ericsson.
 Meneja Miradi wa Zantel Zanzibar Mohamed Ahmed Jaye, akielezea waandishi wa habari (hawapo pichani), jinsi mitambo mipya ya Zantel inavyofanya kazi. Zantel imeanza mradi mkubwa wa kuborersha mtandao wake nchi nzima kwa kufunga mitambo mipya ya mawasiliano kwa ushirikiano na Huawei Technologies na Ericsson.
 Mkuu wa Ufundi wa Zantel Larry Arthur (wa pili kulia) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu uboreshwaji wa mtandao wa Zantel baada ya kuwasili vifaa vipya kutoka Ericsson na Huawei Technologies. Kushoto ni William Cheng (Wei) kutoka Huawei, wa pili kushoto ni Mkuu wa Zantel Zanzibar, Mohamed Khamis Mussa(Baucha), na kulia ni Frode Dyrdal wa Ericsson
 Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa-Baucha (Kulia) akisisitiza jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu  uboreshwaji wa mtandao wa Zantel baada ya kuwasili vifaa vipya kutoka Ericsson na Huawei Technologies. Akimsikiliza ni afisa wa Huawei William Cheng (Wei)
 Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa (kulia) akifurahia jambo na maafisa waandamizi kutoka Zantel, Ericsson na Huawei, baada ya mkutano na waandishi wa habari kuelezea mtandao ulioboreshwa wa Zantel unaoanza kujengwa hivi karibuni. Mradi wa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu.
 Mkuu wa Zantel Zanzibar Mohamed Khamis Mussa (wa pili kulia) na Mkuu wa Ufundi wa Zantel Larry Arthur (wa pili kushoto), wakipongezana na wadau wao wakubwa katika uboreshaji wa mtandao za Zantel unaotarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu ijayo. Kulia ni Frode Dyrdal wa Ericsson na kushoto ni William Cheng wa Huawei.

 Baadhi ya vifaa vipya vilivyowasili Zanzibar kutoka kampuni za Ericsson na Huawei Technologies tayari kwa uboreshaji wa mtandao wa Zantel katika mradi wenye gharama ya zaidi ya Tsh. 2bn/- unaotarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu. Baada ya kukamilika watuamiaji watapata mawasiliano yenye ubora zaidi.
Maafisa waandamizi wa Zantel, Huawei Technologies na Eriscsson, wakiongea na waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali   kuhusu uboreshaji wa mtandao wa Zantel katika mradi wenye gharama ya zaidi ya Tsh. 2bn/- unaotarajiwa kukamilika ndani ya miezi mitatu.

Picha zote na Martin Kabemba

No comments:

Post a Comment

ZanziNews Copyright © 2014

Theme images by Bim. Powered by Blogger.