WACHEZAJI wa Timu ya Yanga ya Tanzania Bara,
wakifanya mazoezi katika uwanja wa michezo Gombani, kwa ajili ya maandalizi ya
mchezo wao dhidi ya Timu ya Simba mchezo huo utakaopigwa Oktoba mosi katika
uwanja wa Taifa wa Tanzania.(Picha na
Abdi Suleiman, PEMBA.)
KOCHA Mkuu wa Timu ya Yanga Hans Van Pluijm, akiwa
katika harakati zake za upangaji wa Koni za kufanyia mazoezi katika uwanja wa
michezo gombani, katika kambi yao ya wiki moja kisiwani Pemba.(Picha na Abdi Suleiman, PEMBA.)
Na Abdi
Suleiman, PEMBA.
BAADA ya
Kuwasili Kisiwani Pemba jana mchana, hatimae mabingwa watetezi wa ligi kuu ya
Tanzania bara timu ya Yanga, imeanza rasmi mazoezi yake leo katika kiwanja cha
michezo Gombani Kisiwani Pemba.
Timu hiyo baada ya kufika kisiwani hapa, iliweza
kwenda moja kwa moja katika hoteli ya Pemba Misali sunset Beachi iliyoko nje
kidogo ya mji wa Chake Chake Wesha, ambako hoteli hiyo imezungukwa na bahari.
Kikosi cha mabingwa hao wa Tanzania bara,
wakiongozwa na kocha wao mkuu Hans Van Pluijin na Kocha msaidizi wa timu hiyo
Juma Mwambusi na viongozi mbali mbali wa timu.
Timu hiyo jana jioni iliweza kufanya mazoezi katika
ufukwe wa bahari iliko hoteli hiyo, kutokana na mazingira yake kuwa tulivu na
ya kuvutia.
Yanga iliweza kufika katika uwanja wa Gombani saa
mbili kamili za asubuhi, kwa ajili ya mazoezi hayo yaliyotumia muda wa masaa
mawili hadi saa nne kamili kumaliza.
Timu hiyo ambayo ipo kisiwani Pemba kwa ajili ya
kujiandaa dhidi ya mahasimu wao wa karibu timu ya Simba katika mchezo wao wa
Oktoba mosi mwaka huu.
Yanga imekuwa na mafanikio mazuri kila inapowasili
kisiwani Pemba, kwa ajili ya kambi yao kutokana na utulivu wa hali ya hewa na
utulivu wa mazingira ya Pemba.
Hata hivyo timu hiyo haikutaka waandishi wa habari
kupiga picha katika mazoezi yao, pamoja na kutokuwa tayari kuzungumza na
waandishi wa habari kutokana na mazoezi yao kufanya siri zaidi.
Mmoja wa viongozi wao kwa masharti ya kutokutaka
kutajwa jina lake gazetini, alisema viongozi wakuu wamekataza waandishi wa
habari kuchukuwa Picha, kwani wataweza kuharibu mipango ya mwalimu.
Alisema timu hiyo itakuwepo kisiwani Pemba kwa muda
wa wiki moja, huku wakitarajiwa kufanya mazoezi siku mbili kwa siku asubuhi na
jioni, ili kuwaweka wachezaji kuwa katika mazingira mazuri dhidi ya michezo yao
ya mbele inayowakabili.
No comments:
Post a Comment